Quantcast
Channel: Francis Godwin ::Mzee wa matukio daima::
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2596
↧

WANAWAKE WAWILI KATI YA WATANO TANZANIA WAMEPATA KUBAKWA TANGU WAKIWA NA MIAKA 15

$
0
0
Wadau wa kupinga masuala ya ukatili wa  kijinsia wakiwa ktk  maandamano  ya  kupinga ukatili  wa  kijinsia





Kijana mkazi  wa Mwangata katika Manispaa ya  Iringa akichezea kichapo baada ya  kukamatwa kwa  tuhuma za kumbaka mtoto  wa miaka 12 hivi karibuni (picha na maktaba ya Francis Godwin Blog)
................................
Taarifa ya Demografia na Afya 2010 ilibaini kuwa wanawake wawili katika kila watano Tanzania wamewahi kukumbwa na ukatili wa kimwili tangu wakiwa na umri wa miaka 15 na mmoja katika kila watano wamewahi kukumbwa na ukatili wa kingono.


 


Mwanaharakati  wa mradi  wa Champion mkoani Iringa Esther Majani anasema  taarifa hizo za hali ya Ukatili wa Kijinsia nchini Tanzania zilitolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (National Bureau of Statistics) kama mojawapo ya vipengele kwenye Taarifa ya Demografia na Afya Tanzania ya mwaka 2010 (Demographic and Health Survey).
Alisema  kuwa  kimsingi  siku hizo pia ni Siku ya Kimataifa ya Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake.

Kauli mbiu ya kitaifa ya Kampeni ya Siku 16 mwaka 2013 ilikuwa ni

FUNGUKA! Tumia mamlaka yako kuzuia ukatili wa kijinsia

na ilimlenga kila mtu kujiangalia jukumu lake kama mhanga, mtenda ukatili na shuhuda katika kupinga ukatili wa kijinsia.



Wadau wa mkoa wa Iringa wanaofanya kazi za kupinga ukatili wa kijinsia na ukatili dhidi ya watoto waliandaa shughuli mbalimbali ndani ya manispaa na wilaya za Mufindi na Iringa Vijijini ambazo zililenga kuijumuisha jamii ya Iringa kufunguka na kuongelea tatizo hili mtambuka.
↧

Viewing all articles
Browse latest Browse all 2596

Latest Images

Trending Articles