Quantcast
Channel: Francis Godwin ::Mzee wa matukio daima::
Viewing all 2596 articles
Browse latest View live

PUNDA WANAVYOSAIDIA USAFIRI VIJIJINI KILOLO M

$
0
0
Mkazi wa  kijiji  cha Ibumu Kilolo akitoka  shamba  kuvuna mazao yake kwa  kutumia usafiri wa punda

MWILI WA BABAKE MBUNGE DEO FILIKUNJOMBE KUSAFIRISHWA LEO KWENDA LUDEWA

$
0
0
Katibu mkuu wa CCM Bw Kinana  kushoto akisalimiana na baba  mzazi wa mbunge  wa  jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe mzee Frolian Filikunjombe ambae amefariki  dunia  juzi akitokea Dubai na mazishi  yake  kufanyika siku ya jumanne wilaya Ludewa leo jumapili mwili  wake  unasafirishwa Kwenda Ludewa

ASAS AMFARIJI MBUNGE FILIKUNJOMBE

$
0
0
kamanda  wa UV CCM mkoa  wa  Iringa Salim Asas  kulia akimfariji mbunge wa  jimbo la Ludewa  Deo Filikunjombe  aliyejishika kichwa kwa msiba wa  babake mzazi leo eneo la Ipogolo mjini Iringa
Asas kulia akimfariji mbunge Filikunjombe leo
Kamanda wa UVCCM mkoa wa Iringa  Salim Asas  kulia akimfariji mbunge Deo Filikunjombe kulia kwa kumpa maji na maziwa ya Asas kwa ajili ya  waombolezaji  wanaokwenda Ludewa katika mazishi mchana  huu
Msanii maarufu  wa Bongo Muvi Keti kulia akiwa na mke wa mbunge Filikunjombe Keti ni mmoja kati ya  wasanii waliopo katika msafara wa  mazishi
Mbunge wa  Ludewa  Deo Filikunjombe katikati akimshukuru Asas kwa kumfariji kushoto ni mbunge wa  jimbo la Mwibara Kang Lugola ambae ni rafriki mkubwa wa Filikunjombe ambae  yupo katika msafara wa waombolezaji ambao wapo katika costa nne kuelekea Ludewa kwa ajili ya mazishi yatakayofanyika siku ya jumanne Ludewa mjini

HABARI KIGANJANI MWAKO UNGANA NASI LEO

MSIBA WA BABAKE FILIKUNJOMBE LUDEWA NI HUZUNI TUPU,ZITTO KABWE KUWASILI KESHO

$
0
0
 Naibu  waziri wa maendeleo ya jamii jinsia na watoto Pindi  Chana akisalimia wananchi na  wafiwa katika msiba  huo
Wadau  wa mtandao  huu  wakiwa katika msiba
Waombolezaji  wakiwa nyumbani kwa  mbunge wa  jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe katika maombolezo
Askari  polisi  wakitoa nyumbani kwa mbunge Filikunjombe mjini Ludewa leo kuungana na  wananchi  kuomboleza
Rafiki mkubwa wa mbunge Filikunjombe Bw Tonny kutoa Marekani kulia akiwa na wanafunzi  wasomi wa  elimu ya  juu katika msiba kutoka  kushoto Basilius Kayombo na Stanley Mkolwe ambao  wanawakilisha umoja wa wana Ludewa wanaosoma vyuo vikuu ambapo Mbunge Filikunjombe ni mlezi  wao
Mbunge Filikunjombe kushoto akiwa na rafiki yake  wakipata msosi
Wananchi  wa Ludewa  wakimiminika nyumbani kwa mbunge Filikunjombe kushiriki maombolezo
Mbunge  Filikunjombe wa pili  kushoto akiwa ameinama chini kwa  huzuni kubwa  baada ya  waombolezaji kufika kumfariji leo kushoto kwake ni mkuu wa wilaya ya Ludewa Juma Madaha na katibu tawala wa wilaya  hiyo
 Msemaji  upande wa Familia ya Filikunjombe mwalimu Dominic Haule  akitambulisha msafara
Rafiki mkubwa wa Filikunjombe mbunge wa  jimbo la Mwibara Kang Lugola akisalimia
Bw Tony akisalimia
Wawakilishi wa  wasomi  wa  vyuo vikuu nchini  wakisema machache
Msomi wa  chuo  kikuu akisalimia
Msanii Kety kutoka Bongo Muvi  akisalimia katika msiba  huo
Eneo la kusaini  kitabu  cha maombolezo

HOTUBA YA NAPE ZANZIBAR

CRDB KAHAMA YATOA MSAADA WA MIFUKO 100 YA SARUJI KWA UJENZI WA ZAHANATI KANGEME ULOWA'

$
0
0
MIFUKO YA SARUJI IKIKABIDHIWA

Na William Bundala(Kijukuu cha bibi k)
Matukio daima Kanda ya ziwa'

KAHAMA
VYAMA vya Msingi vya Wakulima wa zao la Tumbaku Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga vimetakiwa kushirikiana na Taasisi za kifedha yakiwemo Mabenki ili waweze kupata mikopo kwa haraka itakayokuza mitaji yao ya biashara kurejesha kwa wakati ulipangwa.
Meneja Mahusiano wa Benki ya CRDB Kanda ya Ziwa kitengo ya asasi ndogondogo za kifedha Raymond Urassa alitoa Wito huo wakati akitoa masaada wa Mifuko 100 ya Saruji yenye thamani ya shilingi milioni mbili  kwa chama cha msingi cha Tumbaku cha Kangeme Kaya ya ulowa kwa lengo ya kujenga wadi wa Wazazi na akinamama wajawazito katika kata hiyo.
Urassa alisema kuwa Benki ya CRDB kwa sasa imeanza kushirikiana na na vyma vya msingi hasa vile vya wakulima wa zao Tumbaku lengo la kurudisha kiasi kidogo cha sehemu ya faida wanayoipata benki hiyo  katika shughuli za kijamii kwa Wananchi.
Alisema kuwa ili vyma vya msingi viweze kuendelea lazima wakulima washirikiane na kuonyesha umoja wao hasa wakati wa kurudisha Madeni ya Pembejeo wanazozikopo katika taasisi mbalimbali za fedha hususani katika Mabenki.
Pia Meneja Mahusiano huyo aliwataka wakulima kuhakikisha kuwa wanakuwa mstari wa mbele katika kuwadhibiti wale ambao wamekuwa wakitorosha Pembejeo ili kukimbia madeni waliokopeshwa na vyma vya msingi katika eneo husika.
Nae Mgeni Rasmi katika makabidhiano hayo kwa niaba ya Mganga Mkuu wa Halamshauri ya Ushetu John Duttu alisema kuwa msaada huo umekuja wakati muafaka na kuongeza kuwa kutokana na msaada huo ulitolewa na Benki ya CRDB Wananchi katika eneo hilo hawana budi kuhakikisha kuwa wanajenga kwa nguvu zao hadi kufilkia katika lenta hali ambayo Halmashauri ya Wilaya itamalizia  kwa kezeka jingo hilo.
Dr. Duttu aliwataka wakazi wa Ulowa kuhakikisha wanatumia vizuri misaada inayotolewa na Wafadhili mbalimbali kwa nia ya kuleta maendeleo hali ambayo itawafanya watu mbalimbali kuwa ni nia ya kusadia katika maeneo hayo hususani makampuni tumbaku, Asasi za Kibenki pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo.
“Wakulima wa zao la Tumbaku nao wanafamilia zinazowategemea na kwa kupata wodi ya wawazi katika kata hiyo familia zao zitakuwa na afya njema na hata mikopo waliokopa wanaweza kuwa na nguvu ya kuirejesha kwa wakati ulioapangwa”, Alisema Dr. john Duttu katika hafla hiyo.
Kwa upande wake Diwani wa Kata Ulowa Paschal Mayengo alisema kuwa Msaada ulitolewa na Benki ya CRDB utasadia katika kukuza mahusiano mazuri na wakazi wa Kata hiyo na kuongeza kuwa kukamilika kwa Wodi hiyo katika Zahanati hiyo kutanudaisha jumla ya wakazi 25,000 kutoka katika eneo hilo.
 
MATUKIO KATIKA PICHA: 
 

 MENEJA MAHUSIANO WA BENKI YA CRDB KANDA YA ZIWA RAYMOND URRASA MWENYE TISHETI YA MIRABA AKIANGALIA SARUJIA KATIKA GHALA ULOWA.
 AFISA WA BENKI YA CRDB KITOI AKIONGEA NA VIONGOZI WA KATA YA ULOWA BAADA YA KUKABIDHI  MIFUKO 100 YA SARUJI KWA AHILI YA UJENZI WA ZAHANATI KIJIJI HUMO,
 KAIMU MGANGA MKUU WA HALMASHAURI YA USHETU DR. JOHN DUTU AKIONGEA NA VIONGOZI WA KATA YA ULOWA JUZI.
 MFANO WA SARUJI IKIKABDHIWA VIONGOZI WA CHAMA CHA MASINGI CHA TUMBAKU KANGEME ULOWA JUZI.
 HIZI NI KAZI ZINAZOFANYWA NA WAKULIMA WA ZAO LA TUMBAKU BAADA YA MAVUNO KATIKA MSIMU WA MWAKA HUU.

Bi.Asha Bakari Makame


ANDIKENI HABARI ZA KUMKOMBOA MWANANCHI : JAJI BOMANI

$
0
0
DSC_0083

Mshehereshaji ambaye ni Mwanakamati ya maandilizi ya maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014, Usia Nkhoma Ledama akiwatambulisha baadhi ya waandishi wa habari wakongwe (hawapo pichani) kwa mgeni rasmi Jaji Mstaafu Mark Bomani.(Picha zote na Zainul Mzige).

Na Mwandishi wetu

Jaji Mstaafu Mark Bomani amesema lengo la mchakato wa Katiba ni kuhakikisha kwamba Tanzania inapata Katiba ambayo ni bora zaidi kuliko zote itakayoshughulikia changamoto na kuweka mazingira ambayo yatamrahisishia maendeleo mwananchi kwa haraka.

Akitoa risala katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani leo katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa AICC jijini Arusha, Jaji Mstaafu Mark Bomani, amesema jukumu la mwanahabari ni kuwaelimisha baadhi ya wabunge wa Bunge Maalum la Katiba ambao hawana uelewa mkubwa na mchakato wa Katiba hawajui maana halisi ya Katiba mambo ambayo yanasababisha kujadili Katiba hiyo kwa maneno mabaya, kutishiana, matusi na kejeli.

DSC_0171

Baadhi ya waandishi wa habari wakongwe (Ma-veterans) wakimsalimia mgeni rasmi.

“Zoezi la mchakato wa Katiba ni kubwa na wabunge wengi wa Bunge Maalum la Katiba hawaelewi wajibu wao katika kuijadili Katiba hiyo matokeo yake ndio hayo wanayoshuhudia Watanzania”.

Mara nyingi Watanzania wameshuhudia mijadala ya kejeli, malumbano, matusi, kudharauliana pale hoja zinapojengwa na upande ambao haukubaliki na upande mwingine jambo ambalo limewavunja moyo Watanzania na kutokuwa na imani ya kupata Katiba inayolenga kumlinda mwananchi.

Jukumu la wanahabari ni kutoa elimu ya kutosha kuhusu yaliyomo katika Katiba Mpya na kuandika habari za maendeleo ili majadiliano yatokanayo yawe endelevu yamtendee haki mwananchi wa kawaida kwa lengo la kuboresha maisha yao.

DSC_0077

Meza Kuu, kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Elimu, Sayansi na Mawasiliano ya Umoja wa Mataifa (UNESCO) Bw. Abdul Wahab Coulibaly, Mkurugenzi wa Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF) Bw. Ernest Sungura, Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Bw. John Mongela, Mgeni rasmi Jaji Mstaafu Mark Bomani, Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika, Tawi la Tanzania (MISA-TAN), Bw. Mohamed Tibanyendera, Rais wa Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa habari Tanzania (UTPC) Bw. Kenneth Simbaya na Meneja Utafiti na Ushapishaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Bw. John Mirenyi.

“Inasikitisha kuona kuwa hali ya Mtanzania inazidi kudidimia au kubaki pale pale katika sehemu nyingi hasa vijijini katika kipindi cha miaka 40 iliyopita kwa kukosa fursa muhimu za maendeleo na viongozi hawalioni hilo”, amesema Jaji Mstaafu Mark Bomani.

Wakati huo huo mgeni huyo rasmi amekemea tabia ya kuandika habari za kuwasifu viongozi na kupokea Rushwa hali iliyojitokeza katika miaka ya hivi karibuni na kusema kwamba ni fedhea kwa tasnia ya habari kutofuata maadili ya uandishi.

Amesema kwamba nchi itaendeshwa kwa kusimamia haki na ukweli na kuwataka wanahabari wasichoke kuisimamia haki na uhuru wa nchi yao bila woga kwani bila kufanya hivyo nchi itaongozwa kiimla.

DSC_0348

Mgeni rasmi Jaji Mstaafu Mark Bomani, akitoa risala wakati wa maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014 yaliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa AICC jijini Arusha mwishoni mwa juma.

“Kuna tabia ya vyombo vya habari ya vyombo vya habari kununuliwa ili visiandike au kufichua maovu ni fedhea kwani vyombo vya habari ni kioo cha jamii”.

Akizungumzia kuhusu sheria za habari za mwaka 2007 na 2008, Jaji Mstaafu amesema ni aibu kuona mswaada wa sheria ya habari umekwama kwa zaidi ya miaka 10 kwa sababu ambazo hadi leo hazijaeleweka.

Amewataka waandishi wa habari wasikate tamaa na badala yake waendelea na kupambana kuhakikisha kwamba harakati za kupata Sheria ya Haki ya Kujua inafanikiwa ili kupunguza matukio ya manyanyaso, kupigwa, kuteswa, kufungwa kwa vyombo vya habari na kuuwawa.

“Haki haiyombwi simamieni Haki zenu na songeni mbele”, ameongeza Jaji Bomani.

DSC_0429

Sehemu ya wadau wa tasnia ya Habari wakisikiliza risala ya mgeni rasmi.

DSC_0329

Mkuu wa Wilaya ya Arusha, Bw. John Mongela akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa wa Arusha kwenye maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika jijini Arusha kenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa AICC.

DSC_0112

Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika, Tawi la Tanzania (MISA-TAN), Bw. Mohamed Tibanyendera, akizungumza kwenye maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014 yaliyofanyika kwenye ukumbi wamikutano wa Kimataifa wa AICC jijini Arusha.

DSC_0163

Wageni waalikwa na wadau wa tasnia ya habari wakiwa kwenye ukimya kumkumbuka Mwandishi aliyeuwawa mkoani Iringa Daudi Mwangosi.

DSC_0188

Mkurugenzi wa Shirika la Elimu, Sayansi na Mawasiliano ya Umoja wa Mataifa (UNESCO) Bw. Abdul Wahab Coulibaly, akitoa Ujumbe wa Pamoja wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na Mkurugenzi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Irina Bokovas kuhusiana na Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014.

DSC_0217

Meneja Machapisho, Utafiti na Uhifadhi Hati wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Bw. John Mirenyi, akitoa maelezo ya machapisho mbalimbali yaliyoandaliwa na baraza hilo yakiwemo yenye madhila mbalimbali yaliwahi kuwakumba baadhi ya waandishi wa habari ndani na nje ya nchi.

DSC_0241

Mkurugenzi wa Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF) Bw. Ernest Sungura, akizungumzia mchango wa mfuko huo unaowawezesha waandishi wa habari kutafuta habari za uchunguzi na zinazoigusa jamii.

DSC_0247

Wasanii wa Bendi ya Mrisho Mpoto (Mjomba Band) wakitoa burudani kwa wageni waalikwa wakati wa maadhimisho ya siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014 yaliyofanyika jijini Arusha mwishoni mwa juma.

DSC_0156

Sehemu ya wadau wa tasnia ya habari wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri ukumbini hapo.

DSC_0259

Katibu wa Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari nchini (MOAT), Henry Muhanika, akisoma hotuba kwa niaba ya Dr. Reginald Mengi kwenye maadhisho hayo.

DSC_0269

Rais wa Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa habari Tanzania (UTPC) Bw. Kenneth Simbaya, akizungumzia wakati wa maadhimisho hayo.

DSC_0286

Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Absalom Kibanda, akizungumzia changamoto mbalimbali zinazowakumba waandishi wa habari wakati maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014 yaliyofanyika jijini Arusha.

DSC_0288

Mkurugenzi wa TAMWA, Bi. Valerie Msoka, akizungumzia changamoto za usawa wa Kijinsia katika uongozi kwenye Vyombo vya Habari nchini.

DSC_0304

Meneja Uhusiano wa TANAPA, Pascal Shelutete, akizungumzia ushiriki wao kwenye Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014 ambapo aliwataka waandishi wahabari kutumia kalamu zao vizuri katika kukuza Utalii wa Tanzania ndani na nje ya nchi.

DSC_0312

Meneja Uhusiano wa Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro, Bw. Adam Akyoo, akifafanua jambo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014 ambapo amewataka waandishi wa habari kutumia nafasi yao katika kupambana na suala la Ujangili linaloendelea nchini.

DSC_0382

Mrisho Mpoto akiwafungua vitambaa wasaani wa Mjomba Bendi kama ishara ya kuwapa Uhuru waandishi wa Habari kuzungumza kilio chao mbele ya mgeni rasmi kama ujumbe wa Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014.

DSC_0398

Mrisho Mpoto na Bendi yake akighani mashairi na kuelezea madhila wayapatayo waandishi wa habari wawapo kazini ikiwemo usalama wao katika kazi zao za kila siku.

DSC_0405

Makamu wa Rais wa Umoja wa Vilabu vya Waandishi wa habari Tanzania (UTPC), Jane Mihanji akimkaribisha mgeni rasmi Jaji Mstaafu Mark Bomani kuzindua Video mpya ya wimbo "Uhuru Wangu" wa Mrisho Mpoto uliokuwa kwenye Albamu yake mpya inayoitwa WAITE.

DSC_0414

Mgeni rasmi Jaji Mstaafu Mark Bomani, akibonyeza kitufe kuzindua rasmi wimbo huo wakati maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014.

DSC_0422

Wageni waalikwa wakitiza wimbo huo.

DSC_0466

DSC_0497

DSC_0052

DSC_0547

Mkurugenzi wa Mbeya Highlands FM, Bi. Jacqueline Mwakyambiki, akishiriki kwenye maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo Vya Habari Duniani 2014 yaliyofanyika jijini Arusha.

DSC_0445

Mgeni rasmi Jaji Mark Bomani akizindua Album mpya ya Mrisho Mpoto inayoitwa "WAITE".

DSC_0476

Mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani Jaji Mstaafu Mark Bomani akizindua na kuonyesha moja ya Ripoti ya Unyanyasaji dhidi ya Uhuru wa Habari iliyoandaliwa na Baraza la Habari Tanzania (MCT). Kulia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika - Taiw la Tanzania (Misa - Tan), Bw. Mohamed Tibanyendera.

DSC_0493

DSC_0518

MKUU wa Wilaya ya Bagamoyo, mkoani Pwani, Ahmed Kipozi akiteta jambo na mmoja wa Waandishi wa Habari wakongwe Bw. Salim Salim kutoka visiwani Zanzibar.

DSC_0562

Waandishi wa Habari wakongwe (Ma-Veterans) kutoka kushoto Mama Eda Sanga, Fatuma Aloo na Leila Sheikh wakifurahi jambo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yaliyofanyika jijini Arusha .

DSC_0359

Mshauri na Mkufunzi wa Redio Jamii kutoka UNESCO, Mama Rose Haji Mwalimu, akisalimiana na Meneja Uhusiano wa Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro, Bw. Adam Akyoo wakati maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2014 yaliyofanyika jijini Arusha.

DSC_0579

Wadau wa tasnia ya habari wakinunua Album ya msaanii Mrisho Mpoto.

DSC_0572

Baadhi ya wasanii wa Mjomba Band wakiwa kwenye picha ya pamoja na Mwandishi wa habari mkongwe Leila Sheikh.

Mhe. GERVAS KALOLO AFARIKI DUNIA

$
0
0

Aliyewahi kuwa Diwani wa kata ya Miyomboni Kitanzini(CCM) Mhe.GERVAS KALOLO ambaye pia ni Mdau wa KIJIWE CHETU amefariki dunia usiku wa kuamkia leo.

ZITTO KABWE AGEUKA KIVUTIO MAZISHI YA BABAKE FILIKUNJOMBE LUDEWA, CCM WAMTWIKA ZIGO WATAKA ASHIRIKIANE NA MBUNGE WAO KUIBANA SERIKALI BUNGENI UBOVU WA BARABARA NJOMBE- LUDEWA

$
0
0


Kutoka  kushoto mkuu wa wilaya ya  Ludewa  Juma Madah ,mbunge wa  jimbo la Ludewa  Deo Filikunjombe na mbunge wa jimbo la  kigoma kaskazani Zitto Kabwe wakiwa katika msiba wa babake Filikunjombe mjini Ludewa mchana  wa leo
Naibu  waziri wa maendeleo ya wanawake na watoto Pindi Chana na mkuu wa wilaya  ya Njombe Sarah Dumba kulia kushoto ni mwenyekiti wa CCM Ludewa Bw Stanley Kolimba 
Mbunge Filikunjombe  kushoto akifarijiwa
Katibu  wa itikadi na uenezi mkoa wa Njombe Honoratus Mgaya  akimwomba Zitto Kabwe kusaidia kushirikiana na mbunge Filikunjombe juu ya ubovu wa miundo mbinu Njombe- Ludewa
Kamanda  wa polisi Njombe
DC Ludewa Bw Juma Madaha akitambulisha  viongozi mbali mbali
Mbunge Zitto Kabwe  kulia akimfariji mbunge wa Ludewa Deo Filikunjombe leo mjini Ludewa kwa kifo  cha babake mbunge Filikunjombe
Mbunge wa  Ludewa Deo Filikunjombe akiwa na mbunge Zitto Kabwe  kulia
Timu ya wabunge  waliofika  kumfariji Filikunjombe  leo
Mbunge Zitto Kabwe kushoto akishiriki msosi na mbunge Deo Filikunjombe
Mbunge Filikunjombe kulia akiteta jambo na mdogo  wake Philipo ambae  alikuwa akimuuguza babake Dubai na India
RPC Njombe  akiongoza  msafara wa mazishi hayo hii ni polisi jamii ulinzi shirikishi
Mbunge wa  jimbo la Mwibara Kang Lugola akishuka katika gari
Mbunge wa  jimbo la Ludewa  Deo Filikunjombe kushoto  akilitazama jeneza lenye mwili wa babake marehemu  Frolian Filikunjombe likiingizwa  ndani ya kanisa la RC Ludewa kwa ajili ya ibada ya mwisho kabla ya mazishi  yaliyofanyika katika makaburi ya Ludewa mjini
MBUNGE  wa  jimbo la Kigoma Kasikazin Zitto (CHADEMleo amegeuka  kuwa  kivutio  kikubwa  katika mazishi ya babake mbunge wa  jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe huku wananchi  wa  jimbo  hilo na viongozi wa CCM mkoa  wa Njombe  wakimbebesha majukumu  ya ubovu wa barabara  kwa  kumtaka  kushirikiana na mbunge wao  kuwasha moto bungeni .

Zitto  ambae  katika msafara  wake  huo  aliongozana na mbunge wa  jimbo la Mwibara Kangi  Lugola (CCM) mbunge wa  viti maalum mkoa wa  Tanga Amina Mwidau (CUF) na  wengine wa CCM nusuru avuruge  msiba  huo baada ya  wananchi  kuonyesha  kuvutiwa na uwepo  wake na  kumtaka   kusikia  sauti  yake .

Awali  wakati wa utambulisho  wa  viongozi wa kitaifa  uliofanywa na mkuu wa  wilaya ya   Ludewa Juma Madaha  waombolezaji  baada ya  kusikia  jina la Zitto Kabwe  katika orodha ya wabunge hao ndipo  sauti  ziliposikika  kuwa  wanahitaji azungumze .

Hata hivyo  katika  salam  zake katibu wa itikadi na uenezi wa CCM mkoa wa Njombe Honoratus Mgaya mbali ya  kumpongeza  mbunge Kabwe kwa  kufika katika msiba   huo na timu  yake bado  alimtaka  Kabwe na timu  yake  kusaidiana na mbunge  wao Filikunjombe kupigania ujenzi wa barabara ya lami kati ya Ludewa na Njombe.

"Mheshimiwa  Zitto Kabwe wewe ni mmoja kati ya wapiganaji wa kweli  bungeni kama  alivyo mbunge  wetu na jembe  letu wana Ludewa  Deo Filikunjombe ....sasa tunaamini mmeona ubovu wa barabara ya Njombe - Ludewa hivyo  kupitia ninyi  sisi  wana Njombe na Ludewa  tunaomba msaidiane na Filikunjombe kupigania suala la ubovu wa barabara na sio  kutoka nje ya bunge pindi suala la ubovu wa  miundo mbinu linapotolewa na mbunge  wetu"

Kufuatia  ombi hilo la Mgaya  waombolezaji walilipuka kwa  furaha   huku Zitto  Kabwe  akionyesha kuguswa na ombi hilo na kumtania mbunge wa  viti maalum mkoa wa Tanga Amina Mwidau (CUF)  kuwa UKAWA hao .

Zitto Kabwe  ambae alikuwa ni mmoja wa abiria  waliosafiri pamoja na babake Filikunjombe mzee Frolian Filikunjombe kabla ya kufariki  dunia akiwa  ndani ya ndege  kutoka  Dubai kuja nchini ni  mmoja  wa   marafiki  wakubwa wa mbunge Filikunjombe na pia ni mwenyekiti wa kamati ya PAC ambapo  Filikunjombe ni makamu mwenyekiti wake.

Hata  hivyo  alisema  kuwa  ombi la  wana Ludewa  kwake atalifanyia kazi na  kuwa suala la siasa lina  sehemu yake na yanapozungumzwa mambo ya kimaendeleo siasa  za  vyama zinawekwa kando .

Hivyo  alisema  kuwa kutokana na mahusiano mema  kati yake ya mbunge Filikunjombe ameguswa na msiba  huo na kuwa pindi atakapofika  bungeni maombi ya  wana Ludewa atayatendea kazi .

CHAMA CHA MAPINDUZI CHAWAPOKEA RIDHIWANI KIKWETE NA GODFREY MGIMWA HUKO DODOMA

$
0
0
Makamu Mwenyekiti CCM-Taifa Philip Mangula akibadilishana Mawazo na Naibu Katibu Mkuu CCM-Bara Mh:Mwigulu Nchemba na Mbunge wa Chalinze Mh:Ridhiwani Kikwete hii leo wakati wa hafla Fupi ya Kuwapokea Wabunge wapya wa Jimbo la Chalinze na Kalenga,Hafla imefanyika Makao Makuu ya CCM-Dodoma.Mh:Mwigulu Nchemb akimvisha Skafu huyu Mwimbaji baada ya Kuimba nyimbo ya hisia Kuhusu thamani ya Muungano na namna Wapinzani wanavyotaka Kuipeleka Nchi kwenye Utengano na Ubaguzi.
 Mh:Philip Mangula Makamu Mwenyekiti-CCM Taifa akizungumza na Wananchi waliofika Viwanja vya CCM Dodoma Makao Makuu wakati wa Hafla ya Kuwapokea Mh:Ridhiwani Kikwete na Mh:Godfrey Mgimwa.
Mangula ameonya Wana-CCM wanaofanya Kampeni kwenye Majimbo mbalimbali wakati Muda wa Kampeni haujafika,Amesema ni Kosa kwa Mtu yeyote anayejipitisha Kwa Wananchi kuomba ridhaa ya Kugombea Kupitia Chama cha Mapinduzi wakati muda haujafika,Ameomba Jimbo la Kalenga na Chalinze Wabunge wao wapewe nafasi ya Kutekeleza ahadi zao kwa Muda mfupi Uliobakia.Mbali na hilo Philip Mangula ameonya Makundi ndani ya Chama na Usaliti wakati wa Uchaguzi,Mwana-CCM Mtiifu hawezi Kukisaliti chama wakati wowote Ule,Hivyo Ikibainika Umesaliti Chama adhabu yake ni Kali sana.
Baadhi ya Vijana wa CCM-Dodoma Mjini wakipata Picha ya Pamoja na Mh:Mwigulu Nchemba.
 Mh:Mwigulu Nchemba akiongozana na First Lady Mama Salma Kikwete kuelekea kwenye Hafla ya Chakula kwenye Viwanja vya Royal Village Mchana wa leo wakati wa Kuwapokea Mh:Ridhiwani Kikwete na Mh:Godfrey Mgimwa.Burudani zinaendelea.
Mwimbaji Hafsa Kazinja akiwapa Burudani ya Mziki Mh:Mwigulu Nchemba na Wabunge wapya.
 Naibu katibu Mkuu-CCM Taifa Mh:Mwigulu NChemba akifurahia Jambo na Mbunge wa Chalinze Mh:Ridhiwani Kikwete.

Mh:Mwigulu Nchemba akiteta Jambo na Mbunge wa Kalenga Mh:Godfrey Mgimwa.
Dokii akitoa Burudani ya Mziki kwa Wananchi waliofika kwenye tukio hili.
Mh:Ridhiwani akimtambulisha Mke wake Bi.Ridhiwani.
 MH:Ridhiwani Kikwete akitoa neno la Shukrani kwa Wananchi wote na Viongozi wa Chama cha Mapinduzi walioshiriki kwenye Mchakato mzima wa Uchaguzi hadi yeye kufikia hatua hii.
Huyu ndio Mama aliyemlea Ridhiwani Kikwete ndani ya CCM Tangu akiwa na Miaka 6 hadi hapa amekuwa Mbunge wa Jimbo la Chalinze.
Mh:Godfrey Mgiwa akimtambulisha Mke wake.
 Mh:Gofrey Mgimwa akitoa neno la Shukrani kwa Chama cha Mapinduzi na Viongozi wake kwa Kumfikisha hapa baada ya Mchakato Mzito wa Uchaguzi.
Mke wa Mh:Rais Jakaya Mrisho Kikwete-Mama Salma Kikwete akitoa Shukrani kwa Wananchi waliofika kwenye Hafla fupi ya Kuwapongeza Wabunge wapya Mh:Ridhiwani Kikwete na Mgimwa kwa Kuanza safari yao ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano.
Picha/Maelezo na Festo Sanga.

VIDEO:MH:MWIGULU NCHEMBA"SERIKALI MBILI HAZIEPUKIKI,KUNA WAZEE WANATAMANI KUISHI MAISHA YETU WAKATI UMRI HAUWARUHUSU"

$
0
0

Ameyasema haya Wakati wa Hafla Fupi iliyofanyika CCM-Makao Makuu Dodoma kuwakaribisha Wabunge Wapya Kutoka Jimbo la Kalenga Mh:Godfrey Mgimwa na Jimbo la Chalinze Mh:Ridhiwani Kikwete leo Tar.06/05/2014,a

KINANA KUANZA ZIARA YA SIKU 26 TABORA, SINGIDA NA MANYARA

$
0
0
*NI YA KUKAGUA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM
*KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI
* KUKAGUA MAANDALIZI YA CHAMA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye  akiwa na baadhi ya waandishi wa habari watakaoungana na Katibu Mkuu wa CCM, Andulrahman Kinana, katika ziara ya siku 26 katika mikoa ya Tabora, Singida na Manyara itakayoanza kesho katika jimbo la Igunga mkoani Tabora. Nape alipigapicha na na waandishi hao leo baada ya kuzungumza nao kuhusu ziara hiyo, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Mtaa wa Lumumba , Dar eSalaam. Kulia na kushoto ni baadhi ya magari maalum yatakayotumiwa na waandishi hao.

BOMU LALIPUKA LAJERUHI MHUDUMU KANISA LA KKKT MWANZA.

$
0
0

Na Wiliam Bundala matukiodaima.com kanda ya Ziwa (kijukuu cha bibi)
MHUDUMU wa nyumba ya kupumzikia wageni wa Kanisa la KKKT Dayosisi ya Mashariki ya Ziwa Victoria, jijijini hapa, amejeruhiwa vibaya baada ya kulipukiwa na bomu lililokuwa limewekwa kwenye korido la nyumba hiyo.

Tukio hilo lilitokea jana (Jumatatu), kati ya saa 1:45 na saa 2:20 usiku, katika eneo la Makongoro wilayani Ilemela wakati mhudumu huyo Bernadetha  Alfred (25) alipofungua kifurushi cha mzigo alichodhani kimesahaulika kwenye eneo hilo, kabla ya kumlipukia.

Kwa mujibu wa Katibu wa Dayosisi hiyo, Mollel Rogart, kifurushi hicho kilichokuwa kwenye mfuko mweusi wa nailoni, kilikuwa juu ya kreti (tupu) za soda, karibu na eneo la kulia chakula lililopo katika nyumba hiyo.

“Ule mfuko ulikaa pale siku tatu ndiyo usiku huo mhudumu wetu akakichukua kukiangalia akidhani ni mzigo wa mtu umesahaulika.” Alieleza Katibu huyo na kudai kuwa kifurushi hicho kilimlipukia mara tu alipokifungua na kujeruhi vibaya katika sehemu mbalimbali za mwili.

“Bernadetha kajeruhiwa sehemu mbalimbali za mwili ikiwemo miguuni na usoni na siwezi kusema kwamba chanzo cha mlipuko huo ni mambo ya kidini japo ulinzi wetu haukuwa mkali kiasi cha kudhibiti watu walioingia na vitu.” Alisema

Kamanda wa polisi mkoani Mwanza, Valentino Mlowola akithibitisha tukio hilo, alisema kwamba uchunguzi wa awali uliofanywa na kikosi maalum kutoka Dar es salaam umebaini kuwa bomu hilo limetengenezwa kienyeji.

“Bado tunaendelea na uchunguzi wa tukio hilo ili tubaini ni nani kafanya ili kama ni mtu au kikundi kimehusika tuchukue hatua haraka. Natoa wito kwa wananchi kutochukua vitu ambavyo hawa uhakika navyo, wanapoona vitu vya aina hiyo, watoe taarifa kwetu.” Alisema Kamanda Mulowola.

Mlowola alieleza kuwa, Bernadetha aliyejeruhiwa vibaya katika sehemu mbalimbali za mwili, alikimbizwa katika Hospitali ya rufaa ya Bugando ambako anaendelea na matibabu.

Kamanda  huyo alieleza kwamba, mabomu (yakiwemo ya kienyeji) yako katika mifumo mbalimbali hivyo wananchi hususan wahudumu wa sehemu za mikusanyiko wawe na tahadhari na vitu vinavyoonekana kusahaulika na wasisite kuwajulisha polisi vinapoonekana hivyo. 


Mlipuko huo uliozusha hofu kwa waumini mbalimbali wakiwemo wa Kanisa hilo, umetokea ikiwa ni wiki moja baada ya maadhimisho ya ‘Huduma ya Mtoto’ kwa makanisa mbalimbali ya Kikristu jijini hapa yaliyofanyika kwenye kanisa hilo, yakitanguliwa na maandamano kutoka uwanja wa furahisha hadi KKKT.


HOTUBA YA WAZIRI MKUU, MHESHIMIWA MIZENGO PETER PINDA (MB), KUHUSU MAPITIO NA MWELEKEO WA KAZI ZA SERIKALI NA MAKADIRIO YA MATUMIZI YA FEDHA YA OFISI YA WAZIRI MKUU NA OFISI YA BUNGE KWA MWAKA 2014/2015

$
0
0

UTANGULIZI


1.            Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba, kutokana na Taarifa zilizowasilishwa katika Bunge lako Tukufu na Wenyeviti wa Kamati za Katiba, Sheria na Utawala; Kamati ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa; Kamati ya Uchumi, Viwanda na Biashara na Kamati ya Masuala ya UKIMWI zilizochambua Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Bunge lako sasa lipokee na kujadili Taarifa ya Mapitio ya Utekelezaji wa Kazi za Serikali kwa mwaka 2013/2014 na Mwelekeo kwa Mwaka 2014/2015. Aidha, naliomba Bunge lako Tukufu likubali kupitisha Makadirio ya Matumizi ya Fedha ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Taasisi zilizo chini yake pamoja na Ofisi ya Bunge kwa mwaka 2014/2015.

2.            Mheshimiwa Spika, awali ya yote na kwa masikitiko makubwa  naomba  nichukue  fursa  hii kutoa salamu za pole  kwako  na kwa Bunge lako Tukufu kwa kuondokewa na wabunge wawili, Mheshimiwa William Augustao Mgimwa, aliyekuwa Mbunge wa Kalenga, aliyefariki tarehe 01 Januari, 2014 na Mheshimiwa Saidi Ramadhani Bwanamdogo, aliyekuwa Mbunge wa Chalinze, ambaye alifariki tarehe 22 Januari 2014. Aidha, niwape pole Wananchi wa Mkoa wa Mara kwa kifo cha Mheshimiwa John Gabriel Tupa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa huo, kilichotokea tarehe 25 Machi 2014, na kwa Wananchi wa Wilaya ya Urambo kwa kifo cha Mheshimiwa Anna Magowa aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo, kilichotokea tarehe 24 Septemba 2013. Vilevile, natoa pole kwa Wananchi wa Wilaya ya Kalambo kwa kifo cha Mheshimiwa Moshi Mussa Chang’a aliyekuwa Mkuu wa Wilaya hiyo, aliyefariki tarehe 21 Aprili 2014. Naomba pia niwape pole Waheshimiwa Wabunge na  Wananchi  wote  waliofiwa  na ndugu na jamaa zao kutokana na majanga na matukio mbalimbali tangu  nilipowasilisha  Bajeti  yangu  ya  mwaka  2013/2014.

Tunamwomba Mwenyezi Mungu aziweke roho za marehemu wote mahali pema Peponi. Amina! Nichukue fursa hii pia kuwapa pole Wahanga wote wa majanga mbalimbali yakiwemo mafuriko na ajali za barabarani, na niwashukuru kwa dhati wote waliotoa misaada ya hali na mali wakati wa ajali na maafa hayo.

3.            Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha 2013/2014, Bunge lako Tukufu limepata Wabunge wapya watatu ambao ni Mheshimiwa Yusuf Salim Hussein, Mbunge wa Chambani; Mheshimiwa Godfrey William Mgimwa, Mbunge wa Kalenga; na Mheshimiwa Ridhiwan Jakaya Kikwete, Mbunge wa Chalinze. Nawapongeza kwa kuchaguliwa kuwawakilisha Wananchi katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Nawaomba watumie fursa waliyoipata kwa manufaa ya Wananchi na Taifa kwa ujumla.

MAANDALIZI YA BAJETI


4.            Mheshimiwa Spika, huu ni mwaka wa pili tangu tuanze utaratibu wa Mzunguko mpya wa Bajeti ambao unatuwezesha kukamilisha Mjadala wa Bajeti ya Serikali ifikapo tarehe 30 Juni ya kila mwaka.  Taarifa za awali zinabaini kwamba utaratibu huu umeanza kuonesha mafanikio ya haraka katika utekelezaji wa kazi zilizopangwa. Bajeti hii imeendelea kutayarishwakwa kuzingatia utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi   ya   Chama   Cha   Mapinduzi  ya  mwaka  2010; Awamu ya Pili ya Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umaskini Tanzania (MKUKUTA II); Mpango wa Kwanza wa Maendeleo wa Miaka Mitano wa Mwaka 2011/12 hadi 2015/16; Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025; Malengo ya Maendeleo ya Milenia 2015; na Mfumo wa Tekeleza Sasa kwa Matokeo Makubwa (Big Results Now – BRN). Katika mwaka 2014/2015, Serikali itaendelea kutekeleza miradi ya kipaumbele  iliyoainishwa  kwenye  mipango  hiyo  ya  Kitaifa ili kuleta maendeleo endelevu na ya haraka yatakayowanufaisha Wananchi wa Tanzania.

5.            Mheshimiwa Spika, nawashukuru Wajumbe wa Kamati zote za Kudumu za Bunge lako Tukufu kwa mchango wao mkubwa wakati wa uchambuzi wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara, Mikoa, Wakala, Idara za Serikali Zinazojitegemea na Mamlaka za Serikali za Mitaa. Kazi waliyoifanya ni kubwa na ambayo imetuwezesha kukamilisha maandalizi ya Bajeti ninayoiwasilisha leo. Maoni na Ushauri wao utazingatiwa wakati wa kukamilisha mjadala wa Bajeti ya Serikali na utekelezaji wake.

 

HALI YA SIASA


6.            Mheshimiwa Spika, kwa ujumla hali ya siasa Nchini ni tulivu na Vyama vya Siasa vinaendelea kutekeleza majukumu  yao. Nchi  yetu inapitia kwenye kipindi cha mpito ambapo tunaandika Katiba Mpya itakayoweka mustakabali wa  mwelekeo wa Taifa letu kwa miaka mingi ijayo. Nawasihi Wanasiasa na Wananchi wote kwa ujumla kutoa ushirikiano mkubwa wakati wa maandalizi ya Katiba hiyo ambayo baadaye wananchi wote wataipigia kura ya maoni.  Nawaomba tushindane kwa nguvu ya hoja na si hoja ya nguvu katika kuandaa Katiba hii ambayo itatuongoza sasa na vizazi vijavyo.

7.            Mheshimiwa Spika, katika jitihada za kukuza na kuimarisha demokrasia ya vyama vingi Nchini, Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa imeratibu shughuli za Vyama vya Siasa kwa kuhakikisha kunakuwepo na fursa sawa katika shughuli za siasa Nchini. Hadi Aprili 2014, idadi ya Vyama vya Siasa vyenye Usajili wa kudumu imefikia 21 baada ya Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) kupata usajili wa kudumu mwezi Juni, 2013. Aidha, Chama cha Alliance for Change and Transparency (ACT-TANZANIA), Chama cha Wananchi na Demokrasia (CHAWADE) na Chama cha Maridhiano na Uwiano (CMU) vimepata usajili wa muda. Nirejee wito wangu kwa Viongozi na Wanachama wa vyama vyote vya siasa kuendeleza utamaduni wa kuvumiliana na kutohamasisha siasa za chuki na vurugu ambazo zinaweza kutugawa na kuhatarisha amani, utulivu na umoja wa Taifa letu tulioujenga kwa miaka mingi.

 

ULINZI NA USALAMA


Usalama wa Raia


8.            Mheshimiwa Spika, Nchi yetu imeendelea kudumisha amani na utulivu kama tunu ya Taifa iliyojengwa na kuimarishwa tangu tulipopata uhuru. Katika mwaka 2013/2014, Jeshi la Polisi limeendelea kutekeleza Programu ya Maboresho ya Jeshi na Mkakati wa Kupunguza Uhalifu ambavyo vimeongeza ushirikiano na wananchi. Jeshi hilo limeongeza Vikundi 1,778 vya Ulinzi Shirikishi na kufikia vikundi 6,798 kwa mwaka 2013 kwa Nchi nzima. Vikundi hivyo vimechangia kupunguza vitendo vya uhalifu Nchini kutoka Asilimia 4.3 mwaka 2012 hadi Asilimia 2.8 mwaka 2013 na hivyo kuchangia kupungua kwa makosa makubwa na madogo ya jinai kutoka makosa 566,702 mwaka 2012 hadi makosa 560,451 mwaka 2013.

Mauaji ya Wanawake


9.            Mheshimiwa Spika, pamoja na juhudi zinazofanywa na Serikali kwa kushirikiana na Wananchi katika kuimarisha ulinzi na usalama wa raia, hivi karibuni kumetokea wimbi la mauaji ya kikatili dhidi ya wanawake. Katika kipindi cha Januari hadi Aprili 2014, wanawake wanane (8) wameuawa kikatili katika Kata za Mugango, Etaro, Nyakatende na Nyegina Wilayani Butiama. Uchunguzi uliofanyika umebaini kwamba, mauaji hayo yamefanyika mchana na kwa mtindo unaofanana wa kunyongwa na kanga au kamba na miili yao kufukiwa kwenye mashimo mafupi au kufichwa vichakani. Mara zote walengwa ni wanawake wanapokuwa kwenye shughuli zao za kilimo.

10.         Mheshimiwa Spika, Serikali inalaani vitendo hivyo visivyokubalika katika jamii na itawachukulia hatua kali za kisheria wale wote watakaobainika kuhusika kwa namna yoyote. Serikali imechukua hatua kadhaa za kudhibiti vitendo hivyo vya mauaji ikiwa ni pamoja na kuwakamata watuhumiwa 26 na kati yao 13 wamefikishwa mahakamani.  Vilevile, Jeshi la Polisi limeunda kikosi kazi kwa ajili ya kudhibiti hali hiyo na kufanya mikutano ya kuhamasisha jamii kuhusu kuanzisha na kuimarisha vikundi vya Polisi Jamii. Nitoe wito kwa wananchi wema, wenye upendo na Nchi yetu kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu kwenye vyombo vya usalama ili Sheria ichukue mkondo wake.

 

Ajali za Barabarani


11.         Mheshimiwa Spika, ajali za barabarani zimeendelea kuwa tishio kwa maisha ya watu na mali zao. Takwimu za Jeshi la Polisi zinaonesha kuwa katika mwaka 2013, kulitokea ajali za barabarani 24,480 zilizosababisha vifo vya watu 4,091 na majeruhi 21,536 ikilinganishwa na  ajali 23,604 zilizosababisha vifo vya watu 4,062 na majeruhi 20,037 mwaka 2012.  Kwa upande wa pikipiki pekee, mwaka 2012 zilitokea jumla ya ajali 5,763 na kusababisha vifo 930 na majeruhi 5,532.  Mwaka 2013, zilitokea ajali 6,831 na kusababisha vifo 1,098 na majeruhi 6,578. Aidha, katika kipindi cha Januari hadi Machi, 2014 zimetokea ajali 1,449 na kusababisha vifo 218 na majeruhi 1,304. Ajali hizi ni nyingi na zinasababisha vifo vingi na majeruhi ambao wengi wao ni nguvukazi ya Taifa. Ni vyema ikumbukwe kwamba, Serikali iliruhusu matumizi ya pikipiki kwa nia njema ya kupunguza matatizo ya usafiri hususan maeneo ya Vijijini. Hata hivyo, fursa hiyo imeambatana na changamoto ya ajali nyingi barabarani. Hivyo ni wajibu wa madereva wote kuzingatia sheria za barabarani na kukidhi vigezo vyote vya kuwa na vibali halali vya kufanya biashara hizo pamoja na leseni za udereva. SUMATRA, Jeshi la Polisi, Mamlaka za Serikali za Mitaa, na Mamlaka nyingine zinazohusika zinatakiwa kukaa pamoja ili kuweka mkakati wa kukabiliana na ajali hizo ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kwamba Kanuni za Leseni za Usafirishaji wa Pikipiki na Bajaji za mwaka 2010zinatekelezwa ipasavyo.

Hali ya Mipaka ya Nchi


12.         Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuliwezesha Jeshi la Wananchi wa Tanzania kutimiza majukumu yake ya kulinda mipaka ya nchi yetu na raia wake. Katika mwaka 2013/2014, Serikali imewezesha Wanajeshi wetu kupata mafunzo mbalimbali katika vyuo vya ndani na nje ya Nchi pamoja na kushiriki katika mazoezi ya ushirikiano kikanda. Aidha, Jeshi limeshiriki katika operesheni mbalimbali za kulinda amani zinazoongozwa na Umoja wa Mataifa huko Darfur (Sudan), Lebanon, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Sudan Kusini. Nafurahi kulieleza Bunge lako Tukufu kuwa Jeshi limefanya kazi kubwa, nzuri na kwa weledi mkubwa, nidhamu na kujituma hivyo kuendelea kuipatia heshima kubwa Nchi yetu. Katika jitihada za kuwapatia Askari mazingira mazuri ya kuishi, Serikali imeanza kutekeleza Awamu ya Kwanza ya mradi wa ujenzi wa nyumba za Askari ambapo ujenzi wa majengo 191 kati ya 6,064 unaendelea katika vikosi mbalimbali vya Jeshi Nchini.

Mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa


13.         Mheshimiwa Spika, mwaka 2013/2014 ni wa tatu tangu Serikali iliporejesha utaratibu wa kuwachukua Vijana wanaohitimu kidato cha sita kujiunga na mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa Mujibu wa Sheria. Hadi kufikia mwezi Desemba 2013, jumla ya Vijana 15,167 wamehitimu mafunzo ya JKT wakiwemo baadhi ya Waheshimiwa Wabunge wa Bunge hili Tukufu. Mafunzo hayo yamewapatia vijana hao fursa ya kujifunza juu ya Ulinzi, Usalama na Ukakamavu, Uzalishaji mali, Uzalendo na Umoja wa Kitaifa. Katika mwaka 2014/2015, Serikali itachukua vijana zaidi kujiunga na JKT kwa Mujibu wa Sheria. 

 

SHUGHULI ZA UCHAGUZI, BUNGE, MUUNGANO, MABADILIKO YA KATIBA NA VITAMBULISHO VYA TAIFA

 

Tume ya Taifa ya Uchaguzi


14.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Tume ya Taifa ya Uchaguzi ilisimamia na kuendesha chaguzi ndogo za Wabunge katika Majimbo matatu na Udiwani katika Kata 53 nchini. Chaguzi hizo zimefanyika kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo vifo na baadhi ya Waheshimiwa Madiwani kukosa sifa za kuendelea na nyadhifa hizo. Katika Uchaguzi wa Ubunge uliofanyika katika Jimbo la Chambani - Zanzibar, CUF ilishinda kwa kupata Asilimia 84 ya kura zote. CCM ilipata kura Asilimia 12.4, ADC ilipata kura Asilimia 3.5 na CHADEMA ilipata Asilimia 0.4 ya kura zote. Katika Jimbo la Kalenga – Iringa, CCM ilishinda kwa kupata Asilimia 79.3 ya kura, CHADEMA ilipata kura Asilimia 20.2 na CHAUSTA ilipata kura Asilimia 0.5. Katika Jimbo la Chalinze – Pwani, CCM ilishinda kwa kupata Asilimia 86.61, CHADEMA ilipata kura Asilimia 10.58, CUF ilipata kura Asilimia 1.98, AFP ilipata kura Asilimia 0.59 na NRA ilipata Asilimia 0.25 ya kura zote. Aidha, katika Chaguzi za Madiwani zilizofanyika katika Kata 53, CCM ilishinda viti 40, CHADEMA viti 12 na NCCR – Mageuzi kiti kimoja (1).

15.         Mheshimiwa Spika, Tume ya Taifa ya Uchaguzi inaendelea na maandalizi ya kupata vifaa vya kisasa kwa ajili ya zoezi la kuboresha Daftari la Kudumu la Wapiga Kura. Katika awamu hii ya uboreshaji wa Daftari, Mfumo wa Biometric Voter Registration utatumika tofauti na Mfumo wa awali wa Optical Mark Recognition ambao ulikabiliwa na changamoto nyingi za utendaji. Mfumo huu wa kisasa unawezesha uandikishaji na uchukuaji wa alama za vidole kwa haraka zaidi na hatimaye mwananchi kupatiwa kitambulisho cha kupiga kura kwa muda mfupi. Hii itasaidia sana kuokoa muda na kupata takwimu sahihi za wapiga kura watakaoshiriki kwenye chaguzi.

16.         Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii kuwaomba Viongozi wa Vyama vya Siasa kuhamasisha Wanachama na Watanzania wote wenye sifa kujiandikisha kwenye Daftari hilo na kupata kitambulisho halali cha mpiga kura pale zoezi hilo litakapoanza rasmi.  Aidha, ninatoa wito kwa Wananchi wote wenye sifa kujitokeza kujiandikisha. Ni imani yangu kwamba tukitumia fursa hii kikamilifu tutaondoa malalamiko ya majina ya baadhi ya wapiga kura kutokuwepo kwenye orodha wakati wa chaguzi.  Ni muhimu tukumbuke kwamba ni wananchi wenye sifa tu ndiyo watakaoandikishwa. Katika mwaka 2014/2015, Tume itakamilisha zoezi la kuboresha Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, kusimamia Kura ya maoni kwa ajili ya Katiba Mpya, na kuendelea kutoa elimu ya Mpiga Kura kwa Wananchi.

 

Bunge


17.         Mheshimiwa Spika, kuanzia mwezi Julai, 2013 hadi Aprili 2014, Ofisi ya Bunge imeendesha Mikutano Mitatu ya Bunge na Mikutano mitatu ya Kamati za Bunge. Maswali ya Msingi 410 pamoja na maswali 73 ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu yaliulizwa na Waheshimiwa Wabunge na kujibiwa.  Aidha, Miswada minane (8) ya Sheria ilipitishwa na Bunge. Pia, Bunge limekamilisha ukarabati wa Ukumbi wa Bunge na Miundombinu yake kuwezesha Mkutano wa Bunge la Katiba kufanyika na ujenzi wa Ofisi za Wabunge Majimboni umeendelea kufanyika. Vilevile, Ofisi ya Bunge imewajengea uwezo Wabunge na Watumishi wake kupitia semina mbalimbali katika masuala ya Utawala Bora. Katika mwaka 2014/2015, Ofisi ya Bunge itaendelea kuratibu Mikutano ya Bunge, Vikao vya Kamati za Kudumu za Bunge pamoja na kuimarisha miundombinu na majengo ya Bunge.

 

Muungano


18.         Mheshimiwa Spika, tarehe 26 Aprili 2014, tumeadhimisha Miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.  Miaka 50 kwa lugha yoyote ile siyo kipindi kifupi.  Tumeweza kufika hapa tulipo kutokana na misingi imara ya Muungano iliyowekwa na Waasisi wetu na kuendelezwa na Viongozi walioongoza Taifa letu katika awamu zilizofuatia. Tunajivunia kwamba Muungano wa Tanzania umejengeka kwenye historia ya muda mrefu ya ushirikiano wa watu wa pande hizi mbili. Jamii hizi zina uhusiano wa damu, kifikra na mapambano ya pamoja dhidi ya wakoloni waliotawala kwa vipindi tofauti. Walichofanya waasisi wetu mwaka 1964 ni kurasimisha ushirikiano wetu wa muda mrefu. Nichukue fursa hii kuwashukuru na kuwapongeza Watanzania wote kwa kuadhimisha Miaka 50 ya Muungano. Aidha, ninawashukuru kwa dhati Viongozi wote walioongoza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Zanzibar tangu kuasisiwa kwa Muungano. Kwa namna ya pekee namshukuru Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mheshimiwa Dkt. Ali Mohammed Shein, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa Uongozi wao ambao umezifanya pande mbili za Muungano kuwa karibu zaidi.

19.         Mheshimiwa Spika, tumeadhimisha Miaka 50 ya Muungano tukiwa na takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2012.  Takwimu hizo zinaweka jambo moja wazi kwa Muungano wetu; kwamba zaidi ya asilimia 90 ya Watanzania  wote wamezaliwa baada ya Muungano.  Hivyo, tuliozaliwa kabla ya Muungano ni chini ya asilimia kumi.  Kwa mujibu wa takwimu hizo, Tanzania nzima ina watu 44,926,923.  Kati yao, watu 40,640,425, sawa na Asilimia 90.6 ni wa umri wa siku moja hadi miaka 50.  Kwa upande wa  Tanzania  Bara, idadi  ya  watu  ilikuwa  43,625,354,  kati ya hao, watu 39,456,065 sawa na asilimia 90.5 wamezaliwa baada ya Muungano.  Kwa upande wa Zanzibar kulikuwa na watu 1,303,569, ambapo watu 1,184,360 sawa na asilimia 90.9 wamezaliwa baada ya Muungano.  Takwimu hizo zina maana kwamba, asilimia 90.6 ya watu wote wamezaliwa ndani ya Muungano na nchi wanayoifahamu ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.  Sote tunawajibika kuwatendea haki watu hawa kwa kuulinda, kuuimarisha na kuudumisha Muungano wetu.

20.         Mheshimiwa Spika, tuna kila sababu ya kuadhimisha Miaka hii 50 ya Muungano kwa furaha.  Katika maadhimisho ya mwaka huu, tuliandaa maonesho maalum, makongamano na shughuli nyingine ambazo zilisaidia wananchi kuelimishwa kuhusu masuala ya Muungano. Aidha, kimeandaliwa kitabu maalum kinachoelezea historia, utekelezaji wa mambo ya Muungano, mafanikio, changamoto, fursa na matarajio ya Muungano kwa miaka ijayo.  Kitabu hicho kitatumika kama rejea kwa kizazi chetu na vizazi vijavyo.

21.         Mheshimiwa Spika,tutaendelea kuulinda Muungano wetu kwa nguvu zote tukiwa na uelewa kwamba, katika kipindi cha miaka 50 iliyopita Watanzania wameishi kwa amani na kufanya kazi zao za kujiletea maendeleo wakiwa upande wowote wa Muungano. Tunatambua changamoto zilizopo na tumeweka utaratibu mzuri wa vikao ili kuzitafutia ufumbuzi changamoto hizo. Vikao hivyo vitaendelea kufanyika katika ngazi ya wataalam, Watendaji Wakuu na Viongozi wa Kitaifa. Ni imani yangu kwamba, Muungano huu utaendelea kudumu na watu watapata maendeleo makubwa kwani Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ina fursa nyingi zinazoweza kutumika kwa manufaa ya wote.  Sote tukumbuke kuwa, UTANZANIA WETU NI MUUNGANO WETU, TUULINDE, TUUIMARISHE NA KUUDUMISHA!

 

Mabadiliko ya Katiba


22.         Mheshimiwa Spika, tarehe 30 Desemba 2013, Tume ya Mabadiliko ya Katiba ilikamilisha Rasimu ya Pili ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuikabidhi kwa Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi. Napenda kuishukuru Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyokuwa ikiongozwa na Mheshimiwa Jaji Joseph Sinde Warioba kwa kuandaa Rasimu ya Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Rasimu hiyo imeliwezesha Bunge Maalum la Katiba kuanza mjadala. Nitumie fursa hii kuwashukuru Watanzania wote kwa kutoa maoni yaliyowezesha Tume kuandaa Rasimu hiyo ya Katiba.


23.         Mheshimiwa Spika, Bunge Maalum la Katiba linaundwa na Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wabunge wa Baraza la Wawakilishi na Wajumbe 201 walioteuliwa kwa mujibu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya mwaka 2011. Naomba nitumie fursa hii kuwapongeza Wajumbe wote wa Bunge Maalum la Katiba kwa kupata fursa hii ya kuwawakilisha Watanzania katika kuandaa Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.  Ni dhahiri kuwa dhamana hii ni kubwa sana!

24.         Mheshimiwa Spika, Bunge Maalum la Katiba lilianza kazi rasmi tarehe 18 Februari, 2014 kwa kumchagua Mheshimiwa Pandu Ameir Kificho kuwa Mwenyekiti wa muda wa Bunge hilo. Nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Pandu Ameir Kificho kwa kazi nzuri aliyoifanya ya kulisimamia Bunge Maalum hadi kuwezesha kupatikana kwa Kanuni za kuliongoza Bunge hilo. Aidha, niwapongeze Mheshimiwa Samwel John Sitta kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti na Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kuwa Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba. Nampongeza Katibu wa Bunge la Katiba Bwana Yahaya Hamadi Khamis na Naibu wake Dkt. Thomas Kashililah pamoja na Wajumbe wote waliochaguliwa kuwa Wenyeviti na Makamu Wenyeviti wa Kamati 12 za Bunge Maalum. Baada ya kukutana kwa muda wa siku 67, Bunge Maalum limeahirisha Mkutano wake tarehe 25 Aprili, 2014 ili kupisha majadiliano ya Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2014/2015. Ni matumaini yangu kwamba, Bunge Maalum la Katiba litakaporejea litakamilisha kazi hiyo kwa umakini na kupata Rasimu ambayo hatimaye itapelekwa kwa wananchi kwa ajili ya kura ya maoni.

Vitambulisho vya Taifa


25.         Mheshimiwa Spika,katika hotuba yangu ya Bajeti ya mwaka 2013/2014 nilielezea dhamira ya Serikali ya kutoa Vitambulisho vya Taifa kwa Wananchi wake. Napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba, Serikali imekamilisha usajili na utambuzi wa watu kwa upande wa Zanzibar, Watumishi wa Umma na vyombo vya Ulinzi na Usalama pamoja na wakazi wa Mkoa wa Dar es Salaam. Serikali pia, imekamilisha ujenzi wa vituo vya kuingiza na kuhakiki taarifa, kituo cha kutengeneza Vitambulisho na kuhifadhi kumbukumbu pamoja na kituo cha uokozi na majanga ya taarifa na takwimu. Katika mwaka 2014/2015, Serikali itaendelea  na zoezi la Utambuzi na Usajili wa Watanzania katika Mikoa mingine ili kwa pamoja tuweze kunufaika na Vitambulisho vya Taifa katika nyanja za kijamii, kiuchumi na kiusalama.

 

Sensa ya Watu na Makazi


26.                 Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Serikali imeendelea kutoa machapisho mbalimbali ya matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012. Machapisho hayo yanajumuisha Taarifa ya Mgawanyo wa Watu kwa Maeneo ya Utawala; Mgawanyo wa Watu kwa Umri na Jinsia na Taarifa za Msingi za Kidemografia, Kijamii na Kiuchumi. Taarifa hizo zimebaini kuwa, katika miaka kumi iliyopita kumetokea mabadiliko makubwa ya kiuchumi na kijamii katika nchi yetu. Kiwango cha watu wanaojua kusoma na kuandika kimeongezeka kutoka asilimia 69 mwaka 2002 hadi asilimia 78 mwaka 2012. Aidha, uandikishaji halisi katika shule za msingi umeongezeka kutoka  asilimia 69 mwaka 2002 hadi 77 mwaka 2012. Idadi ya watu wanaoishi kwenye nyumba zenye kuta imara ni asilimia 74 na asilimia 65.4 wanaishi kwenye nyumba zilizoezekwa kwa bati. Hata hivyo, pamoja na mafanikio hayo,


hali ya utegemezi nchini ni kubwa kutokana na ukweli kuwa kati ya Watanzania Milioni 44.9, Asilimia 50.1 ni watoto wenye umri chini ya miaka 18. Aidha, takwimu zimebainisha kuwa Asilimia 7.7 ya Watanzania ni watoto yatima. Kutokana na hali hiyo, ni jukumu letu kama Taifa kuweka mipango madhubuti ya kukabiliana na changamoto hizo katika sekta za huduma za jamii ili hatimaye kila mwenye uwezo wa kufanya kazi achangie ipasavyo katika kukuza uchumi na maendeleo ya nchi yetu.

 

MASUALA YA UCHUMI

 

Hali ya Uchumi


27.         Mheshimiwa Spika, Pato la Taifa katika mwaka 2013 lilikua kwa Asilimia 7.0 ikilinganishwa na ukuaji wa Asilimia 6.9 mwaka 2012. Ongezeko hilo limetokana na ukuaji mzuri wa shughuli za huduma za mawasiliano, viwanda, ujenzi na huduma za fedha. Kutokana na ongezeko hilo, wastani wa Pato la Mtanzania limeongezeka kutoka Shilingi 1,025,038 mwaka 2012 hadi Shilingi 1,186,424 mwaka 2013, sawa na ongezeko la Asilimia 15.7. Mfumuko wa Bei umepungua kutoka Asilimia 9.8 Machi 2013 hadi Asilimia 6.1 Machi 2014. Kupungua kwa mfumuko wa bei kumechangiwa na kupungua kwa kasi ya kupanda bei za bidhaa na vyakula hasa mahindi, mchele na aina nyingine ya nafaka.

28.          Mheshimiwa Spika, pamoja na uchumi wetu kukua kwa kasi ya asilimia 7.0 kwa mwaka 2013 na Pato la Mtanzania kuongezeka, kiwango hicho siyo kikubwa sana kuwezesha umaskini wa wananchi kupungua kwa kasi.  Utafiti wa kitaalam unaonesha kwamba, ili umaskini upungue kwa kasi kubwa, uchumi unatakiwa kukua kwa zaidi ya Asilimia 8 kwa kipindi cha miaka 10 mfululizo.  Ukuaji huo pia unatakiwa kulenga Sekta ambazo zinagusa maisha ya watu wengi, hususan kilimo, mifugo na uvuvi. Mwelekeo wa Serikali ni kuweka mazingira wezeshi kwa Sekta za kipaumbele kukua kwa kushirikisha Sekta Binafsi.

 

Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano


29.         Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano 2011/2012 – 2015/2016 ambao unatekelezwa katika kipindi cha mwaka mmoja mmoja. Katika mwaka 2013/2014, Serikali ilitekeleza Mpango huo kupitia Kauli mbiu ya Tekeleza Sasa kwa Matokeo Makubwa. Msingi wa kauli mbiu hii ni kuainisha maeneo  machache  ya  kimkakati  na  kuyatengea  rasilimali za kutosha, kusimamia na kufuatilia utekelezaji kwa karibu zaidi. Chombo maalum cha Ufuatiliaji wa Utekelezaji  wa  Miradi  ya  kimkakati   chini  ya  Ofisi ya Rais kinachojulikana kama President’s Delivery Bureau– (PDB) kimeanzishwa na Watendaji Wakuu wameteuliwa. Ninapenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba, matunda ya utekelezaji wa Mfumo huo yameanza kuonekana katika maeneo makuu sita ya kipaumbele kitaifa ambayo ni Nishati ya Umeme, Uchukuzi, Kilimo, Elimu, Maji na Ukusanyaji wa Mapato.  Utekelezaji wa miradi hiyo na mafanikio yaliyoanza kupatikana yatatolewa maelezo na Mawaziri katika Sekta husika.

Maendeleo ya Sekta Binafsi na Uwekezaji


30.         Mheshimiwa Spika, njia ya uhakika ya kuliwezesha Taifa kuwa na uchumi imara na wa kisasa utakaohimili ushindani katika masoko ya Kikanda na Kimataifa ni kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji. Katika kufikia azma hiyo, tarehe 31 Januari, 2014 nilizindua rasmi Taarifa ya Tathmini ya Sera, Sheria na Kanuni mbalimbali zinazosimamia Uwekezaji Tanzania. Mapendekezo ya Taarifa hiyo yatatumika kuihuisha Sera ya Taifa ya Uwekezaji ya mwaka 1996 pamoja na Sheria ya Uwekezaji Tanzania ya mwaka 1997. Aidha, ili kuwawezesha Wawekezaji na Wafanyabiashara kupata huduma  na taarifa zote muhimu kama vile Sheria, Kanuni na Taratibu mbalimbali kuhusu biashara na uwekezaji kwa njia ya mtandao, Serikali imezindua upya Tovuti ya Kituo cha Uwekezaji Tanzania.  Kupitia Tovuti hii, Wawekezaji popote  duniani  wanaweza  kupata  taarifa kuhusu usajili wa  Kampuni  na  viwango  vya  kodi  kwa  njia  ya mtandao.

Dhamira ya Serikali ni kuboresha mazingira ya uwekezaji na kupunguza gharama za kufanya biashara nchini ili kukabiliana na ushindani mkubwa kutoka nchi nyingine zilizotekeleza maboresho ya mifumo yao ya udhibiti wa biashara.

31.          Mheshimiwa Spika, Sekta Binafsi inaendelea kupewa nafasi kubwa katika kukuza uchumi Nchini. Takwimu zinaonesha kwamba, Miradi iliyosajiliwa na Kituo cha Uwekezaji Tanzania imeongezeka kutoka 869 yenye thamani  ya Shilingi Bilioni 31.5 mwaka 2012 hadi miradi 885  yenye  thamani  ya  Shilingi  Bilioni 141.2 mwaka 2013.
Napenda pia kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba Nchi nyingi duniani zinaendelea kuiamini Tanzania kama Kituo maarufu cha uwekezaji Duniani. Mwezi Novemba, 2011 nilizindua Mpango wa Ushirikiano kati ya Tanzania na Uingereza unaojulikana kama Partnership in Prosperity. Mpango huo umelenga kuongeza uwekezaji kutoka Sekta Binafsi ya Uingereza kwenye mafuta na gesi, kilimo na Nishati jadidifu. Lengo ni kuongeza uwekezaji kutoka Nchi hiyo kwa zaidi ya maradufu ya kiwango cha sasa. Aidha, tumekubaliana kushirikiana kuimarisha mazingira ya biashara ili kurahisisha uwekezaji katika sekta hizo.

32.          Mheshimiwa Spika, baadhi ya Kampuni za Uingereza tayari zimeanza kutekeleza makubaliano hayo kwenye Sekta ya kilimo.  Kampuni ya Unilever kwa mfano, itawekeza zaidi ya Shilingi Bilioni 275 kwenye kilimo cha chai kwa kushirikiana na wakulima wadogo. Tayari Kampuni hiyo imeanza kupanua Kiwanda cha Chai Kibwele, Mufindi na kufungua zaidi ya Hekta 300 za mashamba ya chai katika Wilaya ya Mufindi. Aidha, Kampuni hiyo imeingiza nchini vipando 250,000 vya miche bora ya chai. Pia, Kampuni inaandaa zaidi ya miche milioni 2 kwa ajili ya kuwagawia wakulima wadogo Wilayani Njombe ili waongeze uzalishaji wa chai Nchini.

33.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014,Kituo cha Uwekezaji kimeshirikiana na Uongozi wa Mikoa mbalimbali Nchini kuratibu maandalizi ya Makongamano ya Uwekezaji yenye lengo la kuhamasisha, kukuza na kutangaza fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo kwenye Mikoa hiyo. Jumla ya Mikoa 11 imeshiriki kikamilifu kuandaa na  kufanikisha  Makongamano  ya Uwekezaji katika maeneo yao. Mikoa hiyo  ni  Mwanza,  Mara, Kagera, Geita, Simiyu, Shinyanga, Tabora, Manyara, Tanga, Kilimanjaro na Arusha. Makongamano hayo yamechangia kwa kiasi kikubwa kuzitangaza fursa za uwekezaji zilizopo kwenye Mikoa hiyo, pamoja na kuihamasisha Mikoa na Halmashauri za Wilaya ndani ya Mikoa hiyo kuainisha na kutenga maeneo kwa ajili ya uwekezaji. Aidha, Wawekezaji wengi walioshiriki kwenye Makongamano hayo wameonesha nia na utayari wa kuwekeza kwenye Mikoa husika. Jitihada hizi zitaendelezwa katika kipindi kijacho.

Majadiliano na Sekta Binafsi


34.Mheshimiwa Spika, kwenye hotuba yangu ya Bajeti mwaka 2013/2014, nilieleza kuhusu Mkutano wa Kimataifa wa Majadiliano ya Ushirikiano kwa Manufaa ya Wote. Mkutano huo ulifanyika kuanzia tarehe 28 Juni hadi tarehe 1 Julai 2013, Jijini Dar es Salaam chini ya Uenyekiti wa Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mkutano huo ulitoa fursa ya kipekee kwa Viongozi wa Serikali kujadiliana na kupata maoni ya makundi mbalimbali ya Wananchi kuhusu mbinu za kuongeza kasi ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Serikali imedhamiria kufanya Majadiliano ya Ushirikiano kwa Manufaa ya Wote kila mwaka kuanzia ngazi ya Wilaya, Mkoa hadi Taifa kwa kuzingatia fursa kubwa za maendeleo shirikishi zilizopo kwenye maeneo husika.

35.Mheshimiwa Spika, Baraza la Taifa la Biashara lilifanya Mkutano wake wa Saba tarehe 16 Desemba 2013 chini ya Kauli Mbiu ya “Ukuaji Shirikishi wa Uchumi”. Maazimio ya Mkutano huo ni pamoja na kuunda Kamati Tatu ambazo zitashughulikia Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, Mazingira Wezeshi ya Biashara na Matumizi Endelevu ya Maliasili za nchi. Kamati ya Mazingira Wezeshi ya Biashara imeanza kuishauri Serikali kuhusu mikakati ya kuwavutia wawekezaji wa ndani na nje na kuongeza ushindani  wa bidhaa za Tanzania. Kazi hiyo imefanyika kwa utaratibu wa Maabara chini ya Mfumo wa Tekeleza Sasa kwa Matokeo Makubwa. Utaratibu huo ulianzisha maeneo sita muhimu ambayo yakishughulikiwa yataboresha mazingira ya biashara nchini. Maeneo hayo ni kuboresha Kanuni na Taasisi zinazosimamia biashara; upatikanaji wa ardhi na haki za umiliki wake na kuimarisha ukusanyaji wa kodi na kupunguza wingi wa kodi  na tozo mbalimbali. Maeneo mengine ni kuzuia na kupambana na rushwa; kuboresha Sheria za Kazi na kuimarisha mafunzo na stadi za kazi pamoja na kusimamia utekelezaji wa mikataba na utawala wa sheria.  Katika mwaka 2014/2015, Baraza la Taifa la Biashara litaendelea kuratibu utekelezaji wa maazimio hayo ya Mkutano wa Saba sanjari na kusimamia mikutano ya Mabaraza ya Wilaya na Mikoa.

UWEZESHAJI WANANCHI KIUCHUMI


36.         Mheshimiwa Spika, dhamira ya Serikali ya kubuni na kutekeleza Sera ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ya mwaka 2004 ni kuhakikisha kwamba Watanzania wananufaika na rasilimali  za nchi yao badala ya kubaki kuwa watazamaji.Kwa  kutambua  umuhimu wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi, katika Mwaka 2013/2014Serikali imeanzisha Taasisi  ya  Ujasiriamali na Ushindani wa Kibiashara (Tanzania  Entrepreneurship Competitiveness Centre). Taasisi hiyo itatekeleza jukumu la kutoa miongozo ya uandaaji wa mitaala ya ujasiriamali katika ngazi tofauti na kuhamasisha uzalishaji wa bidhaa bora zitakazohimili ushindani. Aidha, Serikali imeendelea kusimamia Mifuko ya Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na kuongeza ufanisi wake. Hadi kufikia mwezi Februari 2013, Mfuko wa Uwezeshaji wa Mwananchi ulikuwa umepokea Shilingi Bilioni 2.1 zilizotumika kudhamini mikopo ya wajasiriamali kupitia Benki ya CRDB kwa makubaliano ya kukopesha mara tatu ya dhamana ya Serikali. Kutokana na makubaliano hayo, hadi kufikia mwezi Desemba 2013, mikopo yenye thamani ya zaidi ya Shillingi Bilioni 9.5 ilikuwa imetolewa kwa Wajasiriamali 9,790 waliojiunga kwenye Vikundi 283 na Vyama vya Akiba na Mikopo (SACCOS) 51 katika Mikoa 12 na Wilaya 27.

37.         Mheshimiwa Spika, Kwa upande wa Mfuko wa Kuendeleza  Wajasiriamali  Wadogo  na wa Kati, hadi kufikia Desemba 2013,  ulikuwa  umetoa  mikopo  yenye thamani ya  Shilingi  Bilioni  36.39  kwa  Wajasiriamali  62,720. Aidha, Mfuko wa  Maendeleo ya Vijana ulikuwa umetoa mikopo kwa  Vijana  yenye  thamani  ya  Shilingi  Bilioni  1.22 kupitia SACCOS 244; na Mfuko  wa  Maendeleo ya  Wanawake  ulikuwa  umetoa  mikopo  yenye  thamani  ya  Shilingi   Bilioni   5.44  kwa  Wanawake  500,000  Nchini. Vilevile, Mradi wa Mikopo kwa Wajasiriamali Wadogo (SELF) ulikuwa umetoa mikopo yenye thamani ya Shilingi Bilioni 57.1 kupitia Asasi 375 za Kifedha ambapo Wajasiriamali 95,034 walinufaika.

 

Mfuko wa Maendeleo ya Jamii – TASAF


38.Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Awamu ya Tatu ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF III) inatekeleza Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini zilizo katika Mazingira Hatarishi Tanzania Bara na Zanzibar.  Katika kutekeleza Mpango huo, utaratibu wa uhawilishaji fedha kwa kaya maskini ulifanyika katika Mamlaka za Serikali za Mitaa 22 ambapo kaya 138,032 katika Vijiji na Shehia 1,179 zilitambuliwa na kuandikishwa katika Mfumo wa Masijala wenye walengwa 464,552. Hadi sasa, Shilingi Bilioni 5.5 zimehawilishwa katika kaya hizo. Lengo ni kuziwezesha kaya hizo kupata chakula na kujiongezea fursa ya kipato.

39.         Mheshimiwa Spika,Serikali pia imejenga uwezo kwa Viongozi na Wataalam kutoka maeneo ya utekelezaji wa Mpango huo. Uwezo umejengwa kwa kutoa mafunzo katika masuala ya utambuzi, uandikishaji na ukusanyaji taarifa za kaya maskini. Aidha, mafunzo ya usanifu wa miradi ya ujenzi yalitolewa kwa wataalam kutoka Mamlaka za Serikali za Mitaa. Pia, Wajumbe 17 wa Baraza la Wawakilishi na Wakuu wa Mikoa na Wilaya kutoka Zanzibar walitembelea Vijiji vya Pongwe-Kiona na Malivundo (Bagamoyo) na Gwata (Kibaha) ili kujifunza kuhusu utekelezaji bora wa Mpango huo. Katika mwaka 2014/2015, Serikali itaendelea kufanya utambuzi na uandikishaji wa kaya maskini kufikia maeneo yote 161 ya utekelezaji wa Mpango Tanzania Bara na Zanzibar. Lengo ni kutambua na kuandikisha Kaya 920,000 kutoka Vijiji, Mitaa na Shehia 9,000.

 

UZALISHAJI MALI

 

Uzalishaji wa Mazao


40.         Mheshimiwa Spika, hali ya upatikanaji wa chakula ni ya kuridhisha katika maeneo mengi nchini kufuatia mavuno mazuri ya msimu wa 2012/2013. Uzalishaji wa mazao ya chakula kwa msimu huo ulikuwa Tani Milioni 14.38 ikilinganishwa na mahitaji ya chakula ya Tani 12.15 kwa mwaka 2013/2014 ikiwa ni ziada ya Tani Milioni 2.3 za chakula. Ongezeko hilo limefanya Taifa kujitosheleza kwa chakula kwa Asilimia 118 na hivyo, kufanya wastani wa bei za mazao ya chakula katika masoko Nchini kuwa za chini katika kipindi chote cha mwaka 2013/2014.

Ruzuku ya Pembejeo za Kilimo


41.         Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea na juhudi za kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara kulingana na Mipango inayotekelezwa chini ya Kaulimbiu ya KILIMO KWANZA, na Mpango wa Tekeleza kwa Matokeo Makubwa Sasa. Katika mwaka 2013/2014, Serikali imesambaza jumla ya vocha za ruzuku 2,796,300 zenye thamani ya Shilingi Bilioni 83 kwa ajili ya mbolea na mbegu bora za mpunga na mahindi kwa Kaya 932,100. Pia, Serikali ilitoa ruzuku ya dawa za korosho kiasi cha lita 158,845 na Tani 620 zenye thamani ya Shilingi Bilioni 1.5. Vilevile, ruzuku ilitolewa kwa ajili ya uzalishaji wa mbegu bora za pamba Tani 4,000 zenye thamani ya Shilingi Bilioni 4.8, miche ya kahawa 350,000 yenye thamani ya Shilingi Milioni 100 na miche ya chai 1,850,000 yenye thamani ya Shilingi Milioni300.

42.         Mheshimiwa Spika, ongezeko la tija katika uzalishaji wa mazao unategemea sana huduma bora za ugani kwa wakulima. Serikali katika mwaka 2013/2014, ilitoa kibali cha kuajiri Maafisa Ugani 1,452 ili kufanikisha kufikiwa kwa malengo ya kuwa na Afisa Ugani wa Kilimo mmoja kwa kila kijiji. Vilevile, Serikali imeongeza Mashamba Darasa kutoka 16,330 yenye wakulima 344,986 mwaka 2012/13 hadi 16,543 yenye wakulima 345,106 mwaka 2013/2014  ili kuimarisha utoaji wa mafunzo kwa wakulima.

43.         Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kushirikisha Washirika wa Maendeleo kuchangia Programu ya Kuendeleza Kilimo katika Ukanda wa Kusini mwa Tanzania (SAGCOT). Miongoni mwa malengo ya Programu hiyo ni kuwaunganisha wakulima wadogo na mnyororo wa thamani wa kibiashara wa Makampuni makubwa ya ndani na nje ya nchi. Ili kufikia lengo hilo, Serikali imeanzisha Mfuko Chochezi wa Uendelezaji wa Kilimo katika Ukanda wa Kusini mwa Tanzania (SAGCOT Catalytic Trust Fund). Mfuko huo utatoa mitaji itakayogharamia hatua za awali za miradi inayotoa tija ya haraka ambayo imebainishwa kwenye Mpango Mkakati wa Uwekezaji. Vilevile, Mfuko huo utahamasisha biashara inayolenga kumuinua Mkulima mdogo kwa kumuunganisha na mnyororo wa thamani na kampuni kubwa kupitia madirisha makuu mawili. Dirisha la kwanza ni Matching Grant Fund  linalolenga kuwezesha kampuni kubwa zilizoanzisha biashara ya Kilimo Nchini, kuimarisha minyororo ya thamani inayowahusisha wakulima wadogo zaidi au kuanzisha kilimo cha Mkataba kati ya wakulima wakubwa na wakulima wadogo. Dirisha la pili ni Social Venture Capital Fund, linalolenga kuziwezesha biashara changa na za kati kwenye Sekta ya Kilimo au kuwezesha Kilimo cha mkataba kati ya wakulima wakubwa na wakulima wadogo. Tayari Bodi ya Mfuko imeteuliwa na Mtendaji Mkuu wa Mfuko ameajiriwa.

44.          Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Serikali kupitia Mfumo wa Tekeleza Sasa kwa Matokeo Makubwa, inategemea kuvutia uwekezaji na kuanzisha Kilimo cha mashamba makubwa 25 ya Kilimo cha kibiashara kwa mazao ya mpunga na miwa kwa utaratibu wa kuwaunganisha wakulima wakubwa na wadogo wanaozunguka mashamba hayo. Aidha, itaanzisha, itaboresha na kuendesha kitaalamu maghala 275 ya kuhifadhi mahindi kwa kuwaunganisha wakulima katika umoja wa kibiashara kwa ajili ya kupata masoko ya pamoja.

 

Umwagiliaji


45.         Mheshimiwa Spika, katika juhudi za kuendeleza Kilimo cha umwagiliaji Nchini, Sheria ya Umwagiliaji Namba 5 ya mwaka 2013 imeanza kutumika Mwezi Januari, 2014. Sheria hiyo itaiwezesha Serikali kuanzisha Tume ya Umwagiliaji ambayo ni chombo cha kitaifa chenye dhamana ya kusimamia, kuendeleza na kudhibiti shughuli za Umwagiliaji Nchini. Sheria hiyo pia itaanzisha Mfuko wa Taifa wa Umwagiliaji utakaosaidia kutekeleza mipango ya umwagiliaji kwa kulipia gharama za umwagiliaji zinazofanywa na mkulima mmoja mmoja na wawekezaji kupitia mikopo na dhamana. Serikali pia iliendelea na ujenzi na ukabarati wa skimu 24 za umwagiliaji zilizopo katika wilaya 15 Nchini. Katika mwaka 2014/2015, Serikali itaendeleza Skimu za Umwagiliaji 39 kwa ajili ya Kilimo cha mpunga.

Miundombinu ya Masoko ya Mazao


46.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Serikali kupitia Programu ya Miundombinu ya Masoko, Uongezaji Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini imekarabati kilometa 352 za barabara za vijijini kwa kiwango cha changarawe katika Halmashauri za Iringa Vijijini, Njombe Vijijini, Singida Vijijini, Mbarali, Lushoto, Same, Mbulu, Msalala na Mpanda. Halmashauri nyingine ni Maswa, Songea Vijijini, Rufiji, Karatu na Kwimba. Vilevile, imejenga maghala matano yenye uwezo wa kuhifadhi tani 1,000 za mazao kila moja katika halmashauri za Iringa Vijijini, Njombe Vijijini, Same, Songea na Mbarali na kukarabati maghala matatu katika Halmashauri za Sumbawanga, Mbulu na Kahama. Aidha, Programu hiyo imezijengea uwezo benki tisa za wananchi/ushirika ili kuimarisha mfumo wa kifedha Vijijini.

47.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Serikali kupitia Programu hiyo imepanga kukarabati kilometa 434 za barabara kwa kiwango cha changarawe, kujenga maghala 14 na masoko saba katika Halmashauri 64 za Tanzania Bara na Wilaya 10 za Zanzibar. Aidha, wazalishaji wadogo  kutoka Mikoa 24 ya Tanzania Bara na Mikoa mitano ya Zanzibar watajengewa uwezo wa kuhifadhi mazao na mbinu za kufikia masoko ambapo zaidi ya wananchi 100,000 watanufaika na mafunzo hayo.

Maendeleo ya Ushirika

 48.         Mheshimiwa Spika, Sheria ya Ushirika Namba 6 ya mwaka 2013 imetungwa na imeanza kutumika Mwezi Januari, 2014. Sheria hiyo itawezesha kuanzishwa kwa Tume ya Maendeleo ya Ushirika ambayo itakuwa na majukumu ya kusimamia moja kwa moja Vyama vyote vya Ushirika. Aidha,  kupitia Sheria hiyo, Serikali imetoa Waraka Namba 1 wa mwaka 2014 unaotoa ufafanuzi kuhusu Chaguzi katika Vyama vya Ushirika. Ili kuondoa migogoro ya kimaslahi, Waraka huo umewaondoa Viongozi wa Siasa na Serikali katika uongozi wa  Vyama vya Ushirika katika ngazi zote. Katika mwaka 2014/2015, Serikali itaimarisha uratibu wa Vyama vya Ushirika kulingana na mahitaji ya Wananchi na kuunganisha Vyama vya Ushirika na Taasisi za fedha ili kuboresha utoaji wa huduma za kifedha kwa Vyama vya Ushirika.
 

Maendeleo ya Sekta ya Mifugo


49.         Mheshimiwa Spika, kupitia Mpango wa Ruzuku ya dawa ya kuogeshea mifugo, Serikali ilitoa jumla ya lita 11,020 zenye thamani ya Shilingi Milioni 181.8 na kusambazwa nchini. Vilevile, ilitoa chanjo kwa ajili ya kudhibiti magonjwa ya mifugo ambapo dozi 150,000 za chanjo ya Ugonjwa wa Homa ya Bonde la Ufa zenye thamani ya Shilingi milioni 119 ilitolewa katika Mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Manyara, Tanga na Dodoma. Vilevile, Serikali imeimarisha Kituo cha Uhamilishaji kilichopo katika eneo la Usa River, Arusha pamoja na Vituo vingine vitano vya Kanda kwa kusimika mitambo ya kuzalisha kimiminika cha naitrojeni na kujenga Vituo vitano vya madume bora. Vilevile, ng’ombe walionenepeshwa wameongezeka kutoka 132,246 mwaka 2011/2012 hadi kufikia 175,000 mwaka 2013/2014. Ili kuboresha upatikanaji wa maziwa Nchini, Serikali imeongeza uzalishaji mitamba katika mashamba yake kutoka mitamba 943 kwa mwaka 2012/2013 hadi mitamba 1,046 mwaka 2013/2014 na kusambaza Mbuzi wa maziwa 9,530 kupitia Mpango wa Kopa Mbuzi lipa Mbuzi. Jitihada hizi, zimesaidia wafugaji kuongeza tija na hivyo kuchangia ongezeko la uzalishaji wa maziwa kutoka lita Bilioni 1.9 mwaka 2012/2013 hadi lita Bilioni 2 mwaka 2013/2014.

50.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Serikali itatoa ruzuku ya dawa za kuogesha mifugo na kununua dozi milioni moja kwa ajili ya chanjo ya ugonjwa wa Homa ya Bonde la Ufa kwa Mikoa ya Arusha, Tanga, Tabora na baadhi ya mikoa katika Kanda ya Ziwa. Vilevile, Serikali itaimarisha Vituo vya uhamilishaji, mashamba ya kuzalisha mifugo bora na yale yanayozalisha mbegu bora za mifugo pamoja na kununua mifugo wazazi.

Maendeleo ya Sekta ya Uvuvi


51.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Serikali kwa kushirikiana na wadau ilihuisha Sera ya Taifa ya Uvuvi ya mwaka 1997 na Sheria ya Uvuvi Namba 22 ya mwaka 2003 ili ziendane na mabadiliko ya kiuchumi, kisayansi na kiteknolojia. Katika kuimarisha ufugaji wa samaki, wakulima 2,604 walipewa mafunzo ya ufugaji bora wa samaki na mabwawa 64 yalichimbwa. Hatua hiyo imeongeza idadi ya mabwawa ya Samaki kufikia 20,198 yenye uwezo wa kuzalisha Tani 3,029.7 za samaki ikilinganishwa na mabwawa 20,134 yaliyokuwepo mwaka 2012/2013.  Vituo vya kuzalisha vifaranga wa samaki kwa wingi kwa kutumia teknolojia ya ndani viliongezeka kutoka kituo kimoja mwaka 2012/2013 hadi kufikia vituo vitano mwaka 2013/2014 vyenye uwezo wa kuzalisha vifaranga bora vya samaki Milioni 10 kwa mwaka. Serikali pia, ilijenga matanki sita yenye lita za ujazo 8,000 kila kimoja kwa ajili ya kuzalisha vifaranga vya samaki.

52.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2014/2015, Serikali itaanzisha Vituo vya kuzalishia vifaranga vya samaki katika maeneo ya Bacho Dareda - Manyara, Hombolo – Dodoma, na Kigoma. Vilevile, itajenga bwawa la kufuga samaki katika Kituo cha Mafunzo ya Kilimo cha Kilimanjaro – KATC; na kutoa ruzuku kwa ajili ya kuchimba mabwawa na kuzalisha vifaranga wa samaki.
 

Ufugaji Nyuki

 53.         Mheshimiwa Spika, Sekta ya ufugaji nyuki imeendelea kuimarika na kuchangia kuongeza ajira na kupunguza umaskini. Mwaka 2013, thamani ya mauzo ya asali nje yalifikia Shilingi Milioni 287.3 ikilinganishwa na mauzo ya Shilingi Milioni  262  mwaka 2012. Katika kipindi hicho, jumla ya Tani 384 za nta zenye thamani ya Shilingi Milioni 4,660 ziliuzwa nje ikilinganishwa na Tani 277 zenye thamani ya Shilingi Milioni 2,583 zilizouzwa mwaka 2012. Nchi zilizoongoza katika ununuzi wa Asali na Nta ya Tanzania ni Ujerumani, Oman, China, Japan, Yemen, India, Ubelgiji, Botswana, Kenya na Marekani. Kutokana na maendeleo haya mazuri katika mwaka 2013/2014, Serikali imetenga maeneo 20 yenye ukubwa wa Hekta 58,445 sehemu mbalimbali Nchini kwa ajili ya hifadhi za nyuki. Aidha, imetoamafunzo kwa wafugaji nyuki 924 na vikundi 49 kutoka Wilaya 12 pamoja na kutoa elimu ya miongozo na sheria za ubora wa mazao ya nyuki kwa wafanyabiashara wa mazao ya nyuki.

54.         Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2013/2014, Tanzania ilishiriki kwenye Kongamano la Ufugaji nyuki lililofanyika Kiev, Ukraine. Katika Kongamano hilo, mazao ya nyuki kutoka Tanzania yalikuwa kivutio kikubwa na yaliwezesha kupata medali ya Banda Bora la Asali kutokana na asali yake kuwa na viwango vya  ubora na  usalama vinavyokubalika Kimataifa. Aidha, kampuni  mbalimbali  zilionesha nia ya kuwekeza kwenye Sekta ya ufugaji nyuki Nchini. Kama ambavyo nimesisitiza mara kwa mara, sekta ya nyuki ina fursa kubwa ya kibiashara hapa nchini na nje ya nchi.  Ni sekta inayoweza kuleta mapinduzi makubwa katika maeneo mengi kwani yanahitajika mafunzo kidogo na vifaa vichache ambavyo vinaweza  kutumika  kikamilifu  kupata  asali  na  mazao yake.  Niendelee kusisitiza kwamba, tuwahimize wananchi katika Majimbo yetu watumie fursa za ufugaji nyuki zinazopatikana katika maeneo yao ili kujiongezea kipato.

 Maendeleo ya Viwanda

 55.          Mheshimiwa Spika, Sekta ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo imeendelea kutoa mchango muhimu katika upatikanaji wa ajira, ongezeko la kipato na ukuaji wa uchumi. Katika mwaka 2013/2014, Serikali imefungua Vituo vya Teknolojia Mikoani kwa ajili kuhudumia Wajasiriamali wanaotengeneza mashine za kusindika mazao na kutengeneza bidhaa mbalimbali za uzalishaji mali. Vituo hivyo vimewezesha kuanzishwa kwa miradi mipya 4,127 ya uzalishaji mali kwenye mikoa ya Lindi, Mbeya, Iringa, Arusha, Kigoma na Kilimanjaro. Aidha, Wajasiriamali 23,546 walipatiwa mafunzo ya ujasiriamali na ujuzi maalum wa ufundi na utumiaji wa mashine za uzalishaji mali. Vilevile, huduma za ushauri na ugani zilitolewa kwa Wajasiriamali 20,769 kwenye Vikundi na Vyama vyao vya Biashara kwa kuviimarisha na kuviwezesha kujenga misingi ya kujitegemea.

56.          Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza Mkakati wa “Wilaya Moja, Bidhaa Moja” kwa kujenga uwezo wa kuzalisha bidhaa kutokana na malighafi zilizopo kwenye Wilaya husika. Kupitia Mkakati huo, Serikali imejenga uwezo wa kuongeza thamani ya mazao na bidhaa mbalimbali, kuzalisha mitambo na vipuri pamoja na zana za kilimo ambapo viwanda vidogo 198 vilianzishwa na kuwezesha upatikaji wa ajira 1,809. Aidha, Serikali inatekeleza Mradi wa Kuendeleza Ujasiriamali Vijijini (MUVI) kwa kutumia dhana ya kuimarisha mlolongo wa thamani kimikoa kwa mazao mbalimbali. Mradi umewezesha uanzishwaji wa miradi midogo 15,580 Vijijini; urasimishaji wa Vikundi 65,308 vya uzalishaji na upatikanaji wa ajira 39,574.

57.         Mheshimiwa Spika, Serikali pia iliendelea na juhudi za kuhamasisha uwekezaji kwenye miradi mipya katika Maeneo Maalum ya Uzalishaji (Export Processing Zones) na Maeneo Maalum ya Kiuchumi (Special Economic Zones). Hadi kufikia mwezi Desemba 2013, kampuni 32 zilikuwa zimesajiliwa na Mamlaka ya EPZ kwa ajili ya kuanzisha viwanda vipya kwenye maeneo hayo. Aidha, Serikali imekamilisha utafiti kwenye Mradi wa Makaa ya Mawe Mchuchuma na kuthibitisha uwepo wa tani Milioni 370 za makaa ya mawe katika eneo la kilomita za mraba 30 kati ya kilomita za mraba 140 zilizotengwa kwa ajili ya Mradi huo. Aidha, utafiti huo ulithibitisha uwepo wa tani Milioni

TAARIFA YA KIMICHEZO TOKA TASWA

$
0
0
WIKI iliyopita kulifanyika Mkutano Mkuu wa Chama cha Kimataifa cha Waandishi wa Habari za Michezo (AIPS) jijini Baku, Azerbaijan.
 
Mkutano huo ulishirikisha viongozi wa vyama 116 vya waandishi wa habari za michezo duniani, ambapo Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), kiliwakilishwa na Katibu Mkuu, Amir Mhando.
 
Katika mkutano huo msisitizo mkubwa umewekwa kwa nchi wanachama kutilia mkazo program za kuwaendeleza waandishi chipukizi wa habari za michezo, lakini pia AIPS yenyewe nayo pamoja na Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Afrika (AIPS-Afrika) vimechukua jukumu la kusaidia kwa wale watakaokidhi vigezo wanavyohitaji.
 
Hivyo kila nchi mwanachama itatuma wasifu wa majina ya wanahabari chipukizi wasiozidi watano, ambao AIPS yenyewe itaangalia wale watakaofaa na kuwaandalia mafunzo baadaye mwaka huu.
 
Kwa upande wa AIPS Afrika yenyewe itaendesha mafunzo kwa wanahabari chipukizi 25, ambayo yatafanyika Morocco, lakini kipaumbele cha kwanza kitakuwa kwa nchi 16 zitakazocheza fainali za mataifa ya Afrika mwakani nchini humo na nafasi zingine zitabaki kwa nchi ambazo hazitaenda Morocco.
 
Mafunzo ni ya wazi kwa waandishi wowote chipukizi wasiozidi umri wa miaka 25, hata wale waliopo kwenye vyuo vya uandishi wa habari wataruhusiwa kuomba. Tanzania imewahi kupata nafasi moja mwaka 2011, ambapo Mwita Mwaikenda wakati huo akiwa mwanafunzo wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, alishiriki mafunzo hayo yaliyoandaliwa na AIPS akiwa miongoni mwa Waafrika watatu tu waliopata nafasi hiyo.
 
Utaratibu kuhusiana na suala hili utaelezwa vizuri baada ya kikao cha Kamati ya Utendaji ya TASWA kitakachofanyika Jumatatu wiki ijayo kujadili masuala mbalimbali.
 
 
B: Ziara Uganda
Kulifanyika kikao cha viongozi wa nchi wanachama wa AIPS ambao wanatoka Afrika Mashariki, ambapo nchi za Burundi, Kenya, Tanzania na Uganda zilishiriki na kukubaliana kufanyike ziara ya kimafunzo itakayohusisha waaandishi wa habari za michezo Septemba 25-29 mwaka huu Kampala, Uganda. Rwanda licha ya kutoshiriki mkutano wa AIPS, lakini tulikubaliana nayo ialikwe.
 
Katika makubaliano hayo kila nchi itakuwa na washiriki wasiopungua 20 na wasiozidi 35, ambapo pia litafanyika kongamano kuhusiana na masuala mbalimbali ya waandishi wa habari za michezo kwa ukanda huo na siku ya mwisho litafanyika bonanza la michezo mbalimbali. Taarifa zaidi za ziara hiyo itatolewa siku za usoni.
 
C; Ushirikiano wa kimafunzo
 Baadhi ya nchi zilizoshiriki mkutano huo wa 77 wa AIPS, zilikubaliana kuanzisha utaratibu wa kubadilishana utaalamu wa kitaaluma kwa nchi mbalimbali, kwa kuwatoa baadhi ya wanahabari kwenda nchi zilizo katika makubaliano hayo kujifunza kwa gharama za nchi mwenyeji.
 
Hata hivyo makubaliano hayo, yataanza kufanya kazi baada ya kila nchi kupata baraka za Kamati ya Utendaji na kutuma majibu kwa waratibu kwamba wanaafiki. Kamati ya Utendaji ya TASWA katika kikao chake kijacho hilo litakuwa moja ya ajenda.
 
Nawasilisha.
 
Katibu Mkuu TASWA
07/05/2014
 
Cio…

BABAKE MBUNGE FILIKUNJOMBE AZIKWA KIFAHARI ZAIDI YA MSANII KANUMBA

$
0
0
Wabunge  wakitoa heshima zao
Msanii wa bongo muvi Kety akitoa heshima za mwisho
Mbunge wa  jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe akitoa heshima zake katika jeneza lenye mwili wa babake mzee Frolian Filikunjombe
Waombolezaji  wakiangua  kilio wakati wa  kutoa heshima  zao

Waziri mkuu mstaafu  Edward  Lowasa akifuatiwa na mbuge wa jimbo la Mwibara Kangi Lugola wakitoa heshima zao
Waziri  wa nchi  ofisi ya  waziri mkuu  sera na uratibu wa  bunge Wiliam Lukuvi akitoa heshima zake kwa mzee Filikunjombe
Mbunge wa kigoma Kaskazin Zitto Kabwe akiongozana na waziri mkuu mstaafu Lowassa na Kangi Lugola kutoa heshima zao
Mbunge  wa  jimbo la Mwibara Kangi  Lugola (CCM) akiwa na mbunge wa Kigoma Kaskazin Zitto Kabwe (Chadema) nyumbani kwa mbunge   Deo Filikunjombe jimboni Ludewa
Mbunge Filikunjombe kulia  akinywa pombe aina ya ulanzi  huku mbunge Kangi Lugola na Zitto Kabwe katikati  wakishuhudia
Mheshimiwa kangi akiuliza pombe hiyo
hapa Mheshimiwa kangi akiketi katika kiti
Mmoja kati ya  wachina akimpa pore  Filikunjombe
Mbunge Zitto kabwe kushoto akimfariji Filikunjombe
Askofu wa RC Njombe Afredy Maluma akiwa na maparoko  wake  wakimsikiliza mbunge wa  jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe
Waombolezaji  wakiwa katika ibada
Jeneza lenye mwili wa babake Deo Filikunjombe
Filikunjombe  kulia akitoka kanisani na Zitto Kabwe na mbunge Amina Mwidau
Jeneza hilo  likiwekwa  eneo la kaburi  tayari kwa  kushushwa kwa mashine kaburini
hapa Jeneza likiwa  limewekwa  juu ya kaburi kabla ya kushushwa kwa mashine
Mbunge Filikunjombe katikati akiwa na familia  yake
vifaa maalum  vikitolewa  ili jeneza  hilo liweze kushushwa kwa mashine kaburini
Jeneza likianza  kushuka kaburini kwa mashine
Jeneza  likishuka kaburini kwa mashine
Jeneza  likiendelea  kushuka kwa mashine sio kwa kamba kama ilivyo kwa msanii Kanumba
Waombolezaji  wakigombea  kupiga  picha wakati jeneza  hilo likishuka kwa mashine kaburini
Jeneza  likiendelea  kushuka kaburini
Waombolezaji  wakipunga mikono ya kwaheri  wakati jeneza likishuka kaburini kwa mashine
Jeneza  likiendelea  kushuka
Jeneza  likipotea potea
hapa jeneza  likimalizikia kushuka kaburini
Baada ya jeneza  kufika mwisho  wake
hapa kamba  za mashine  hiyo  zikitolewa
Jeneza likiwa limetulia  eneo lake ardhini
Waombolezaji  wakijiandaa kuitoa mashine  iliyotumika kushusha jeneza  hilo
Waombolezaji  wakitoa mashine  hiyo
kaburi baada ya  kutolewa mashine  hiyo
Askofu wa RC Njombe Afredy Maluma akitoa baraka  za mwisho
Mbunge wa jimbo la Ludewa Deo Filikunjombe akiweka udongo katika kaburi la babake
Mdogo wa mbunge Filikunjombe Gredo Filikunjombe akiweka udongo
Familia ya Filikunjombe ikiweka udongo
kaburi  likifunikwa kwa mbao na karatasi maalum
Msanii wa bongo muvi  Keti katikati akiwa na mke wa mbunge Filikunjombe Habiba Filikunjombe kulia na  waombolezaji  wengine
paroko akiweka msalaba
Mbunge wa  Ludewa Deo Filikunjombe kushoto na ndugu  zake  wakiweka shada la maua
mama wa Filikunjombe akiweka maua
Watoto wa Falikunjombe  na ndugu  wengine  wakiweka shada la maua
Habari Kamili  itakujia

MAABUSU WAVUA NGUO NA KUKUMBATIA MLINGOTI WA BENDERA YA TAIFA WAKITAKA KESI YAO ISIKILIZWE

$
0
0
Askari polisi wakiwalinda mahabusu wawili kati ya sita wanaotuhumiwa kwa kesi za mauaji, wakiwa wameng'ang'ania mlingoti wa Bendera ya Taifa huku mnoja akiwa mtupu mara baada ya kutoroka toka kwenye msafara wa mahabusu waliokuwa wakiingia mahakama ya wilaya ya Nyamagana na kisha mmoja wao kuvua nguo.
Inspector Henry akiwasihi mahabusu hao wawili wanaotuhumiwa kwa kesi za mauaji, kuachia mlingoti wa Bendera ya Taifa na kurudi kwenye chumba cha mahakama kwaajiri ya taratibu za kesi.
Inspector Henry (shati la bahari) akiwa na Inspector Veda (mwenye koti) wakisikiliza hoja za  Thobiasi Warioba (35), aliyeamua kuvua nguo zote na kubaki mtupu akiwa ameng'ang'ania mlingoti wa Bendera ya Taifa uliopo katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mfawidhi Wilaya ya Nyamagana mkoa wa Mwanza, ambaye anakabiliwa na kesi ya mauaji Na. 32/2012.
Inspector Veda (mwenye koti) akichukuwa maelezo ya Thobiasi Warioba (35), aliyeamua kuvua nguo zote na kubaki mtupu akiwa ameng'ang'ania mlingoti wa Bendera ya Taifa uliopo katika viwanja vya Mahakama ya Hakimu Mfawidhi Wilaya ya Nyamagana mkoa wa Mwanza, ambaye anakabiliwa na kesi ya mauaji Na. 32/2012. akiwa na mwenzake Hamis Ramadani (30).
Ushawishi ukiendelea.
Mahabusu Thobiasi Warioba (aliye mtupu) pamoja na mwenzake Hamis Ramadhani katu katu waking'ang'ania mlingoti wa bendera ya Taifa huku wakishinikiza kuzungumza na waandishi wa Habari.
Wananchi wamefurika viwanja vya mahakama.
Baada ya kuzungumza na waandishi wa habari mahabusu hao walikubali kurejea chumba cha Mahakama.
Nje ya Mahakama kuelekea lango kuu.
Wananchi wamefurika viwanja vya mahakama.
Mashuhuda.

MAHABUSU wawili kati ya sita wanaotuhumiwa kwa kesi za mauaji, wameleta kizaazaa baada ya kujaribu kutoroka na kukimbilia kwenye mlingoti wa Bendera ya Taifa nakuing'ang'ania kisha kuvua nguo na mmoja wao kubaki mtupu.


Tukio hilo limetokea leo majira ya saa 4:00 asubuhi katika Mahakama ya Hakimu Mfawidhi wa Wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza, wakati mahabusu hao walipofikishwa kwa ajili ya kusikilizwa kwa kesi zao, lakini ghafla walipofika kwenye viwanja vya mahakama hiyo walitimua mbiyo kuelekea kwenye mlingoti wa Bendera hiyo ya Taifa na kuvua nguo.

Wananchi waliokuwa katika viwanja vya mahakamani hapo waliachwa midomo wazi na hali ya mshangao, mara baada ya mmoja kati ya hao wawili wakifanikiwa kuufikia mlingoti huo na kuvua nguo kisha kuanza kupiga kelele kwa kupaza sauti kudai haki itendeke.

Tukio hilo pia lilishuhudiwa na watumishi wa Mahakama ya Wilaya, Mahakama ya Mwanzo, Mamlaka ya Maji Safi na Majitaka ya jijini hapa (MWAUWASA), Askari wa Jeshi la Wananchi (JWTZ), na taasisi zingine zilizo jirani na majengo ya mahakamani hapo na wananchi waliokuwa wakisubilia kesi zao kutajwa.

Mahabusu hao sita waliojaribu kutoroka na kuishia kudhibitiwa vyombo vya dola, walitajwa kwa majina kuwa ni Thobiasi Warioba (35), aliyeamua kuvua nguo zote na kubaki mtupu eneo la mlingoti wa Bendera ya Taifa, ambaye anakabiliwa na kesi ya mauaji Na. 32/2012.

Watuhumiwa wengine waliojaribu kutoroka ni Hamis Ramadani (30), Anthony Petro (35), Marwa Mwita (38), na Chacha Wangwe (35), na mwingine ambaye hakufahamika majina yake mara moja, wote wanakabiliwa na kesi ya Jinai Na. 215/2013  na walikamatwa tangu mwaka 2011.

Wakiwa katika viwanja vya mahakama hiyo baada ya kudhibitiwa na askari polisi, mmoja wa mahabusu hao walisikika wakisema: “Haiwezekani, tangu mwaka 2011 tulipokamatwa hadi sasa kesi zetu hazijasikilizwa. Wengine tumebambikiziwa kesi.  “Tunaomba haki zetu, polisi mnatuonea, vyombo vya habari tunaomba mtusaidie  tumekaa muda mrefu bila kusikilizwa na hatujui hatma yetu tangu 2011 tulipo kamatwa tumechoka kukaa mahabusu, tunaomba kesi zetu zisikilizwe”.

Baada ya malalamiko yao, ndipo askari  mmoja aliyejitambulisha kuwa ni Inspekta Henry akiwa na wenzake sita waliokuwa wakiwadhibiti wasikimbie na kuwahoji kuhusiana na madai yao, huku askari hao wakiwataka kuondoka katika mlingoti huo na kumtaka Warioba avae nguo ili waweze kuingia mahakamani.

“Pamoja na maamuzi yenu haya, lakini mtambue mnavunja sheria na hili ni kosa jingine la jinai, hivyo ni vema mkaondoka kwenye mlingoti huu na kuingia mahakamani. Malalamiko yenu tumeyasikia na yatashughulikiwa,” alisema Inspekta Henry.

Mmoja wa maofisa waandamizi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Mwanza, ambaye alikataa kutajwa jina lake, alidai ushahidi wa kesi za watuhumiwa hao bado haujakamilika, na kwamba kesi zao haziwezi kusikilizwa na mahakama ya wilaya kwani haina uwezo na badala yake zitatajwa tu kisha kuhamishiwa Mahakama Kuu.

“Bado hiyo ni Criminal Case (kesi ya mauaji) au PI Case hivyo Mahakama Kuu haiwezi kuzungumzia hilo kwa sasa kwa kuwa utaratibu wa mahakama kuu ikisha kuwa tayari huitwa ‘Criminary Session Case’, ambapo sasa hupangiwa namba ya kesi na Jaji wa kuisikiliza,”  alisema.

RAIS KIKWETE AKUTANA NA WAZIRI MKUU WA CHINA JIJINI ABUJA

$
0
0

 Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akikutana na Waziri Mkuu wa China Mhe. Li Keqiang kwa mazungumzo oembeni ya Mkutano wa Uchumi Duniani kwa bara la Afrika jijini Abuja, Nigeria, Mei 7, 2014

 Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete katika mazungumzo na Waziri Mkuu wa China Mhe. Li Keqiang pembeni ya Mkutano wa Uchumi Duniani kwa bara la Afrika  jijini Abuja, Nigeria, Mei 7, 2014

Viewing all 2596 articles
Browse latest View live